Friday, November 29, 2013

RAIS JAKAYA KIKWETE APEWA UCHIFU BARIADI

D92A6333 
Mmoja wa machifu wa Kisukuma eneo la Bariadi ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Mashariki Andrew Chenge akimvika vazi la kijadi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya kumpa uchifu Rais Kikwete iliyofanyika mjini Bariadi,Mkoa mpya wa Simiyu leo.Rais Kikwete alipewa jina la kisukuma la Chifu Ng’humbu Banhu lenye maana ya 
 
 
 
. D92A6385 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa amekalia kigoda cha Uchifu wa Bariadi baada ya kuwa Chifu Ng’humbu Banhu mjini Bariadi Mkoa mpya wa Simiyu leo.Rais Kikwete yupo katika Ziara ya Kikazi Mkoa mpya wa Simiyu(picha na Freddy Maro)

KINANA AUNGURUMA TUNDUMA

 

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akihutumia maelfu ya wananchi katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mwaka, mjini Tunduma, wilayani Momba, jioni hii, Nov 28, 2013, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi na kuzungumza nao njia ya kuzitatua, katika mkoa wa Mbeya.

 Wananchi wakiwa wamembeba Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakati wa mkutano mkubwa wa hadhara uliohudhuria na maelfu ya wananchi katika uwanja wa shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya, leo
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye 'akihutoa dozi' alipohutubia katika mkubwa wa hadhara uliohudhuria na maelfu ya wananchi katika uwanja wa shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya, leo
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akitoa 'dozi' katika mkutano mkubwa wa hadhara uliohudhuria na maelfu ya wananchi katika uwanja wa shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya, leo
 Dk. Asha-Rose Migiro akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano uliofanyika  Uanja wa shule ya  Mwaka, Tunduma,leo
Katibu wa NEC, Siasa na Uhisiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro (katikati mwenye  miwani) akiselebuka na wananchi kwenye mkutano, Uwanja wa shule ya  Mwaka, Tunduma leo. Imetayarishwa na theNkoromo Blog --

Monday, November 25, 2013

SOMA TAARIFA YA ZITTO KABWE NA DR KITILA MKUMBO BAADA YA KUVULIWA NAFASI ZA UONGOZI NDANI YA CHADEMA

1
Taarifa ya Dk. Kitila Mkumbo kwa Umma kuhusu Kuvuliwa nafasi za mamlaka
ndani ya CHADEMA
1. Katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika tarehe 20-22
Novemba 2013, pamoja na mambo mengine, kulijadiliwa waraka wa siri
unaojulikana kama Mkakati wa Mabadiliko 2013. Waraka huu ulilenga kujenga
hoja ya kufanya mabadiliko ya uongozi na kuanisha mikakati ya ushindi kwa
mgombea mlengwa katika uchaguzi mkuu ndani ya CHADEMA. Nilikiri kuwa
nilikuwa naufahamu waraka huu, na kwamba nilishiriki kuuandaa na kuuhariri, na
kwamba mimi ni mmoja wa wanachama wanaoamini kwamba kuna haja ya
kubadilisha uongozi wa juu wa chama katika uchaguzi ujao ndani ya chama.
 
2. Katika mjadala, maudhui ya waraka huu yalionekana kwa wajumbe kwamba
yalikuwa na mapungufu na yalikiuka misingi na kanuni zilizoanishwa katika
Katiba ya Chama. Kwa kuwa katika chama cha siasa hoja za watu wengi ndizo
hupewa uzito, na kwa kuwa dhamira na nia yangu ndani ya chama hiki imekuwa
ni kusukuma mabadiliko ambayo watanzania wanayatazamia nje ya mfumo wa
sasa wa utawala, nilikiri makosa yangu na kuwaomba msamaha wajumbe wa
Kamati Kuu na viongozi wakuu wa chama, na kueleza kwamba nilikuwa tayari
kujiuzulu na kubaki kuwa mwanachama wa kawaida. Wajumbe walikataa
kukubali ombi langu la kujizulu bali walipitisha azimio la kunivua mimi na Mhe.
Zitto Zuberi Kabwe nafasi zetu za uongozi. Nilipokea kwa unyenyekevu adhabu
ya kuvuliwa nafasi zote za mamlaka nilizokuwa nazo ndani ya chama hiki na
kueleza kuwa nitaendelea kutoa mchango wangu kama mwanachama wa kawaida
hadi hapo chama kitakapoona ninafaa kukitumikia katika nafasi yeyote.
 
3. Kufuatia mkutano wa waandishi wa habari siku ya Ijumaa tarehe 22 Novemba
2013 ambapo, pamoja na mambo mengine, ilielezwa na viongozi wa CHADEMA
kwamba mimi na wenzangu (Samson Mwigamba na Zitto Kabwe) tumehujumu
chama na tumefanya uhaini kwa kuandaa mkakati wa ushindi kwa mgombea
tunayemtaka, ningependa nieleza mambo yafuatayo:
 
a. Siamini hata kidogo kwamba kugombea nafasi yeyote iliyo wazi ndani ya
chama cha siasa ni uhaini na hujuma. Msingi namba moja wa CHADEMA
ni demokrasia na hakuna namna ya kudhihirisha mapenzi kwa demokrasia
zaidi ya kuruhusu ushindani katika nafasi za uongozi na hasa uongozi wa
2
juu kabisa. Hiki kinachoitwa uhaini ni wasiwasi wa siasa za ushindani
katika chama chetu.
 
b. Sijawahi na sitarajii kushiriki vitendo vyovyote vya kuhujumu chama
changu cha CHADEMA na harakati za mabadiliko hapa nchini. Chama
hiki kiliniamini katika nafasi nyingi nyeti sana na kama mie ningekuwa
mhujumu nilikuwa na fursa nzuri za kufanya uhujumu huo. Nimeshiriki
kuandaa ilani ya chama ya 2010-2015, kuratibu kampeni za mwaka 2010
nikiwa makamu mwenyekiti wa kampeni chini ya Profesa Baregu na
nilishiriki kutengeneza na kusimamia utaratibu mzuri wa kupata wabunge
wa viti maalumu katika chama chetu. Zote hizi ni nafasi nyeti mno ambazo
kamwe huwezi kumkabidhi mtu ambaye ni ‘mhaini’ na ‘mhujumu’.
 
Nilishiriki katika shughuli za chama kwa kiwango ambacho
nilijisababishia matatizo makubwa katika familia yangu na kazini, lakini
sijawahi kutetereka na sijaterereka. Nilifanya yote haya kwa mapenzi
yangu ya dhati na imani yangu kwa CHADEMA kwamba ndicho chama
kinachostahili kuongoza harakati za mabadiliko hapa nchini kwa sasa.
 
c. Nasikitika kwamba nimesababisha usumbufu kwa viongozi wangu wa
CHADEMA kutokana na dhamira yangu ya kutaka mabadiliko ya uongozi
ndani ya chama chetu kwa njia halali za kidemokrasia. Nilifanya hivi kwa
imani niliyo nayo kwa misingi ambayo CHADEMA inasimamia, ikiwemo
demokrasia, na imani yangu kwamba chama hiki kinahitaji kufanya
mabadiliko makubwa katika uongozi wa juu wa chama, ikiwa ni
maandalizi muhimu kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Nasisitiza
tena kwamba siamini hata kidogo kwamba matamanio ya mabadiliko ya
uongozi ndani ya chama, na kuandaa mikakati ya kufikia matamanio
hayo kwa njia za kidemokrasia ni uhaini.
 
d. Tunaweza kujifunza kutokana na historia. Siasa za ushindani ndani ya
vyama katika nchi hii sio kitu kigeni. Enzi za TAA na kabla TANU
haijazaliwa wanachama walikuwa wanagawana nafasi za uongozi mezani.
Lakini mwaka TANU ilipozaliwa (mwaka 1954) kulikuwa na uchaguzi
mkali sana kwa nafasi ya uenyekiti. Mwalimu Nyerere alimshinda Mzee
Skyes kwa kura chache sana. Rais Obama wa Marekani alianza mkakati
wa kushinda uteuzi wa kugombea nafasi ya urais kupitia chama chake cha
Democrat mapema kabisa mwaka 2006 kupitia waraka maalumu wa siri
3
ulioainisha mikakati yake. Waraka huu uliandaliwa na watu wanne tu bila
yeye mwenyewe kujua. Waandaji wa mkakati huu walikuja kumshirikisha
baadaye mwaka 2007 na kumshawishi yeye ajitokeze kugombea dhidi ya
Hillary Clinton aliyekuwa anachukuliwa kama mrithi halali wa kiti cha
urais. Yaliyobaki ni historia. Hivi ndivyo ambavyo siasa za ushindani
ndani ya vyama hatimaye huzaa wagombea na viongozi imara katika nchi.
e. Zitto Zuberi Kabwe hajafukuzwa kwa sababu ya waraka huu kwa sababu
yeye hakuhusika kwa namna yeyote kuandaa, ingawa alikuwa ni mlengwa
mkuu. Yeye amefukuzwa kwa sababu ambazo yeye atazieleza na ambazo
viongozi wa CHADEMA hawakuzieleza katika mkutano na waandishi wa
habari.
 
f. Napenda ijulikane kwamba sikuomba kujiuzulu kwa sababu ya kuogopa
aibu ya kufukuzwa. Niliomba kujiuzulu kwa sababu nilitambua kwamba
wenzangu katika Kamati Kuu walikuwa hawana imani nami tena, na ni
uungwana kujiuzulu mkifika mahala hamuaminiani. Nilitambua vilevile
kwamba, kwa mujibu wa Katiba yetu, Kamati Kuu ilikuwa haina uwezo
wa kunivua nafasi yangu moja kwa moja. Kwa mujibu wa Katiba ya
CHADEMA, Sura ya Sita, Ibara ya 6.3.6 (b), inasomeka hivi “Kiongozi
aliyeteuliwa na vikao vya uongozi ataweza kusimamishwa au kuachishwa
uongozi na kikao kilichomteua”. Mimi nilichaguliwa na Baraza Kuu na ni
kikao hiki pekee chenye uwezo wa kunivua nafasi niliyokuwa nayo.
Ninaamini wajumbe wa Kamati Kuu walipitiwa katika hili kwa sababu
siamini kwamba hawajui takwa hili la kikatiba ukizingatia kwamba ndani
yake kuna wajumbe waliobobea kabisa katika tasnia ya sheria.
 
4. Hiki kilichotokea ndani ya chama sio kitu kibaya. Vyama vingi imara hupitia
katika migogoro na misukosuko kama hii na zaidi. Naamini tutavuka na tutakuwa
imara zaidi. Muhimu ni kwamba ni lazima tuaminiane. Katika kuaminiana sio
lazima tufanane kimawazo na kimtazamo kwa sababu hili ni jambo
lisilowezekana kibinadamu na zaidi katika siasa.
 
5. Ninapohitimisha, ninawasihi wanachama wa CHADEMA na wapenzi wa
mabadiliko popote walipo wapiganie kwa dhati MISINGI mama ya CHADEMA
ikiwemo demokrasia ndani ya chama. Hakuna namna ambavyo chama chochote
kinaweza kushawishi umma kwamba kitapigania demokrasia katika nchi wakati
kinayahainisha mapambano ya kidemokrasia ndani ya chama chenyewe.
4
Kukataa siasa za ushindani ndani ya chama ni kuhujumu demokrasia na ni
usaliti kwa misingi mama ya chama ambayo ni uhuru wa kweli na mabadiliko
ya kweli. Hisia za usaliti na umamluki zilitumika enzi za ukomunisti katika
kunyamazisha wapinzani ndani ya vyama vya siasa na katika nchi. Zilikuwa ni
njia haramu zilizozoeleka ambazo hatimaye zilizaa udikteta wa kutisha katika
mataifa ya kikomunisti. Tusikubali utamaduni wa kuhisiana usaliti na umamluki
ukaota mizizi katika chama chetu na katika nchi kwa sababu utaua demokrasia na
mfumo wa vyama vingi utakuwa hauna maana tena.
 
6. Nitafuata taratibu zote za chama kama zilivyoelekezwa na Kamati Kuu na kwa
mujibu wa katiba yetu, na nitashiriki kikamilifu katika kutuliza hali ya kisiasa
ndani ya chama ili kuhakikisha kwamba tunabaki imara, na CHADEMA
inaendelea kuwa tumaini la watanzania.
Mungu ibariki Tanzania.
Dkt. Kitila Mkumbo
Dar es Salaam
Jumapili, 24 Novemba 2013.

mheshimi Zitto kabwe akisalimiana na wazazi wake mama na babawaliofika kumsikiliza



wazazi wa mheshimi Zitto kabwa baba yake na mama yakena dada yake

wandishi wa habari waliofika katika mkutano wa zitto na kitila leo


TAARIFA YA ZITTO ZUBERI KABWE (MB) KUHUSU KUVULIWA NAFASI ZA
UONGOZI NDANI YA CHAMA CHANGU CHA CHADEMA
1. Utangulizi
i. Katika kikao chake cha siku mbili kilichofanyika tarehe 20 22
Novemba 2013            ,
Kamati Kuu ya CHADEMA, pamoja na mambo mengine, iliazimia kunivua
nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama. Kwa mujibu wa taarifa ya chama
iliyotolewa katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Ijumaa tarehe 22
Novemba 2013, ilielezwa kwamba sababu za kuvuliwa uongozi mimi na Dk
Kitila Mkumbo ni uhaini na hujuma kwa chama kutokana na waraka unaojulikana
kama mkakati wa uchaguzi 2013.
 Ukweli ni kwamba waraka uliotajwa si sababu
ya mimi kuvuliwa nafasi zangu za uongozi kama ilivyojadiliwa katika Kikao cha
Kamati Kuu . Sababu za kufukuzwa kwangu kama zilizojadiliwa katika kikao cha
Kamati Kuu ni tuhuma lukuki ambazo si mara yangu ya kwanza kuzisikia
zikijadiliwa ndani na nje ya vikao vya chama. Hitimisho la tuhuma hizi ni kwamba
mimi nimekuwa nikikisaliti chama kwa kutumika na CCM na Usalama wa Taifa.
Nitazianisha tuhuma hizi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika
vikao mbalimbali vyama.
 
ii. Ninatambua kwamba chama changu kinapita katika wakati mgumu sana sasa
hivi. Nataka nitamke mapema sana kwamba mimi Zitto Zuberi Kabwe sitokuwa
chanzo cha CHADEMA kuvunjika. Hiki ndicho chama kilichonilea na kunifikisha
hivi nilivyo. Ningependa chama hiki mtoto wangu atakapokuwa mtu mzima na
atakapoamua kujiunga na siasa aingie CHADEMA. Bado nina imani kubwa na
chama changu na ninaamini ndicho kinachostahili kuendesha nchi jana,
leo na kesho.
 
2. Kuhusu tuhuma mbalimbali zinazo elekezwa kwangu
Zipo tuhuma nyingi ambazo zimekuwa zikirudiwarudiwa katika vikao vya chama na
nje ya vikao na baadhi ya viongozi wenzangu. Tuhuma hizi zinalenga kuonyesha
kwamba mimi ni mbinafsi na kwamba ninapokea rushwa ili kukihujumu chama
changu. Nitazianisha tuhuma kwa kifupi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa
2
  nikizijibu katika vikao mbalimbali vya chama.
i) Tuhuma kwamba sikushiriki kumpigia kampeni mgombea wetu wa urais katik          a
uchaguzi wa mwaka 2010. Ningependa kueleza yafuatayo kuhusu jambo hili:
Mimi nilikuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Kaskazini huko Kigoma.
Pamoja na kuwa mgombea wa ubunge, nilifanya kampeni katika majimbo mengine
16 katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Dar es Salaam, Mtwara, Pwani, Shinyanga,
Mara na Rukwa. Hakuna kiongozi yeyote wa juu aliyefanya kampeni katika majimbo
mengi kama mimi, ukiacha mgombea urais.
 
Kote nilipopita nilimpigia kampeni wagombea wetu wa udiwani, ubunge na Rais.
Katika Mkoa wa Kigoma nilizunguka na mgombea urais katika kata zote za Kigoma
Kaskazini na majimbo yote manane ya Mkoa wa Kigoma.
ii) Tuhuma kwamba katika Mkoa wa Kigoma nilishindwa kuwapigia kampeni
wagombea wetu kiasi kwamba peke yangu ndiye niliyeshinda katika uchaguzi huo.
Ukweli ni kwamba niliwapigia sana kampeni wagombea wetu, na hivyo ndivyo wapiga
kura wa Kigoma walivyoamua.
 
iii) Tuhuma kwamba nilishiriki kuwashawishi wagombea wetu katika baadhi ya
majimbo kujitoa katika uchaguzi wa mwaka 2010 ili kuwapisha wagombea wa CCM
wapite bila kupingwa kwa njia ya rushwa. Majimbo yanayotajwa ni pamoja na
Sumbawanga, Musoma Vijijini na Singida Mjini. Kama nilivyokwisha kueleza katika
vikao mbalimbali vya chama jambo hili si la kweli na hakuna popote ambapo watoa
tuhuma hizi wamewahi kutoa ushahidi kwamba nilifanya jambo hili. Nipo tayari kwa
uchunguzi ndani ya chama na watoa tuhuma waje na ushahidi bayana wa jambo hili. Si
afya kwa chama kuendelea kurudiarudia tuhuma hizi kila mara tangu mwaka 2010 bila
uchunguzi wowote kufanyika na jambo hili lifikie mwisho.
 
iv) Tuhuma kwamba nimekuwa sishiriki katika operesheni mbalimbali za chama: Ukweli
ni kwamba nimeshiriki sana katika operesheni mbalimbali za chama ndani na nje ya
nchi. Kwa mfano, mwaka 2011 tulikuwa na operesheni kubwa katika mikoa ya Kanda
ya Nyanda za Juu Kusini na nilikwenda katika mikoa yote tuliyotembelea. Mwaka 2012
3
baada ya hoja ya mkonge bungeni nilifanya ziara Mkoa wa Tanga. Mwaka 201            2
kulikuwa na operesheni kubwa moja katika mikoa ya kusini ya Mtwara na Lindi.
Operesheni hii sikushiriki kwa sababu nilikuwa nchini Marekani kufungua matawi kwa
mwaliko wa Watanzania wanaoishi huko.
 
v) Tuhuma kwamba nimekidhalilisha chama kwa tamko la PAC kwamba Hesabu
za Vyama hazijakaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
(CAG): Katika jambo hili ninatuhumiwa kwamba mimi kama Naibu Katibu
nilipaswa kuwasiliana kwanza na viongozi wa chama 'kuwatonya' ili wajiandae.
Kwamba kutokuwatonya kumekidhalilisha chama na kukiweka kundi moja na CCM na
nastahili kuadhibiwa vikali kwa kuwa katika taarifa yangu nilikuwa na nia mbaya na
chama chetu. Maelezo yangu niliyoyatoa na ambayo ningependa kuyakariri hapa
kuhusu jambo hili ni kama ifuatavyo:
 
Utawala bora hautaki mimi kutumia nafasi yangu ya uenyekiti wa PAC kulinda
chama changu na kuonea vyama vingine. Kufanya hivyo ni kuendeleza tabia zile zile
ambazo tunazipinga na ambazo tunapigania kuzibadilisha
Napenda kusisitiza kwamba hakuna chama ambacho kimewahi kukaguliwa na
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG). Natambua kwamba mahesabu ya
chama changu yamekuwa yakikaguliwa na wakaguzi wa nje kwa utaratibu
tuliojiwekea. Lakini matakwa ya kisheria ni kwamba mahesabu ya vyama vya siasa
hayajakaguliwa na CAG, na hili ni kosa la kisheria, bila kujali kosa hili ni la nani.
vi) Tuhuma kwamba mimi ni mnafiki katika kukataa kwangu kuchukua Posho
za Vikao
Mtakumbuka kwamba mimi nilikataa kuchukua posho tangu mwaka 2011 kama ishara
ya kuonyesha kwa vitendo msimamo wa chama chetu wa kupinga posho za kukaa na
matumizi mengine yasiyofaa katika fedha za umma kama ilivyoanishwa kwenye Ilani
yetu ya mwaka 20102015.
 
Mtakumbuka kwamba hivi karibuni Mheshimiwa Lema
amenishutumu kwamba kukataa kwangu kuchukua posho ni unafiki kwa sababu
ninapokea posho kubwa zaidi katika mashirika ya umma ambapo mimi ni mwenyekiti
wa kamati husika. Ninapenda kueleza yafuatayo kuhusu jambo hili:
Sipokei posho yeyote ya vikao (sitting allowance) ndani na nje ya Bunge tangu
4
mwaka 2011. Hii ni pamoja na vikao vyote katika Kamati za Bung           e
ninavyohudhuria. Mtu yeyote mwenye ushahidi vinginevyo auweke hadharani.
Swala la kukataa posho (sitting allowance) ni swala la kiilani katika chama chetu, na
kwangu ni swala la kimisingi zaidi. Katika Wilaya yangu vifo vya kina mama
wajawazito ni 1900 kati ya wanawake 100,000 wenye ujauzito. 
Vifo hivi vinatokana
na ukosefu wa huduma kwa sababu ya bajeti finyu. Ndiyo maana nilifurahi sana kwa
chama chetu kuliweka swala la kupunguza matumizi ya Serikali katika Ilani, na
kuondoa posho za wabunge, ambao tayari wanapokea mishahara mikubwa,
kungesaidia sana kupatikana fedha ambazo zingeokoa vifo vingi vya kina mama.
Jambo hili si suala la ugomvi baina yangu na Mheshimiwa Lema. Ni suala la
msingi katika chama chetu.
 
3. Usambazaji wa Ripoti ya Siri kuhusu Zitto Kabwe
Hivi karibuni kulisambazwa waraka unaoitwa ripoti ya siri kuhusu mimi ukibeba lundo la
tuhuma kwamba nimehongwa fedha nyingi ili kukihujumu chama changu. Waraka huu
ulidaiwa kuwa umechomolewa kutoka makao makuu ya CHADEMA. Jambo hili pia
lilijadiliwa katika kikao cha juzi kwa kifupi, na majibu ya viongozi wa chama ilikuwa ni
kwamba waraka huu haukuandaliwa wala kusambazwa na makao makuu. Katika
mchango wangu nililalamikia mambo matatu yafuatayo:
 
i. Kwamba baadhi ya waliokuwa wanasambaza waraka ule walikuwa ni viongozi wa
chama chetu. Bahati mbaya hadi leo hakuna hata mmoja ambaye
amekwishachukuliwa hatua za kinidhamu. Ninaamini kwamba kuna siku watu hao
watachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za chama chetu.
 
ii. Kwa kuwa chama kimekana rasmi kuhusika na waraka huu, nitaendelea na taratibu
za kisheria ili kuhakikisha kwamba wote waliohusika kutengeneza hekaya ile
wanachukuliwa hatua stahiki za kisheria.
 
4. Hitimisho
a) Ninatambua kwamba kuna watu walitegemea leo ningejibu mapigo na
ningewazodoa watu kwa majina kama ilivyo kawaida katika siasa za Tanzania.
Natambua pia kwamba, kama ilivyo kawaida wakati wa migogoro katika vyama vya
5
siasa hapa Tanzania, kuna watu walitegemea leo ningetangaza 'maamuzi magumu'         .
Natambua kwamba wapo ambao wangependa kupata nafasi ya kuendelea
kutumia suala hili katika harakati zao za kudhoofisha mapambano ya
demokrasia na uthabiti wa siasa za ushindani nchini mwetu. Napenda
wanachama wa CHADEMA na wapenda demokrasia na siasa safi wote nchini
watambue kwamba mimi bado ni mwanachama mwaminifu wa chama hiki na
nitakuwa wa mwisho kutoka kwenye chama hiki kwa hiari yangu. Nitafuata taratibu
zote ndani ya chama katika kuhitimisha jambo hili.
 
b) Naomba wanachama waelewe kwamba mimi kama binadamu ninaumia
ninapopigwa. Tuhuma ninazorushiwa ni kubwa na zinanikwaza. Tuache siasa za
uzushi ili tujenge chama chetu na nchi yetu, ili hatimaye tuwakomboe Watanzania
wenye matarajio na imani kubwa kwa chama chetu.
 
c) Kama mwanasiasa kijana niliyekaa katika siasa kwa muda sasa yapo mengi
mazuri nimeyafanya. Lakini kuna maeneo nilipojikwaa na yapo makosa
niliyofanya kisiasa katika maisha yangu ya siasa.
 
d) Kinachoendelea ndani ya chama chetu ni mapambano ya kukuza demokrasia. Ni
mapambano baina ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina, waumini wa
uwajibikaji dhidi ya wabadhirifu na wapenda siasa safi dhidi ya watukuzao siasa
majitaka. Hii ni changamoto kubwa ndani ya chama chetu inayohitaji uongozi
shupavu kuikabili. Nitasimama daima upande wa demokrasia. Kama alivyopata
kunena mmoja ya wanasiasa maarufu, 'kiwango cha juu kabisa cha uzalendo katika
nchi ni kukubali kutofautiana kimawazo', na ninatamani huu ndio uwe utamaduni wa
chama chetu.
Kabwe Zuberi Zitto, Mb
Dar es Salaam.
24 Novemba, 2013
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...