Saturday, June 21, 2014

WATU SITA WAMEFARIKI PAPO HAPO KATIKA AJALI BARABARA YA BAGAMOYO ENEO LA MAKONGO JIJINI DAR ES SALAAM

BAADHI YA WATU WALIOPOTEZA MAISHA KUTOKANA NA AJALI HIYO

HALI ILIVYOKUWA ENEO LA AJALI

MOJA YA BASI LILOHUSIKA KATIKA AJALI

HII NDIYO HALI HALISI ENEO LA AJALI

ENEO LA AJALI

Watu sita wamekufa papo hapo na wengine 12 wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari manne yakiwemo mawili ya abiria iliyotokea eneo la Makongo barabara ya bagamoyo jijini Dar es Salaam leo saa saba mchana.

Walioshuhudia ajali hiyo wamesema imetokea wakati dereva wa gari la abiria lililokuwa likielekea Mwenge kutoka Tegeta ambaye alikuwa katika mwendo wa kasi kubwa kushindwa kulimudu gari lake na kusababisha kuhamia upande wa pili wa barabara na kuligonga basi lingine la abiria lililokuwa likitokea Mwenge kuelekea Tegeta.

Akielezea ajali hiyo,kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa kipolisi kinondoni kamanda AWADH HAJI amesema ajali hiyo ilitokea saa saba mchana na kuhusisha magari manne moja likiwa la raia wa China ambalo liliwakanyaga majeruhi na kuwaua sita kati yao.

Mganga Mkuu wa hospiitali ya jeshi Lugalo ambako maiti na majeruhi walipelekwa brigedia jenerali Dr Makere Josiah amethibitisha kupokea majeruhi kumi na wawili na maiti sita huku wengine hali zao zikiwa mbaya na kukimbizwa hospitali ya taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.

TAZAMA PICHA ZA BABU SEYA NA MWANAE PAPII KOCHA WAKITUMBUIZA KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAGEREZA

NGUZA VICKING AKILICHARAZA GITAA HUKU PAPII AKIIMBA

PAPII KOCHA AKICHEZA KWA MADAHA




PAPII KOCHA AKIIMBA HUKU BABA YAKE NGUZA VICKING AKIPIGA GITAA KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAGEREZA YALIYOFANYIKA KATIKA BWALO LA MAGEREZA SIKU YA IJUMAA 20/06/2014 DAR ES SALAAM

PAPII AKITUMBUIZA NA WAFUNGWA WENZIE

PAPII AKIIMBA KWA HISIA WIMBO MAALUM WA SIKU YA MAGEREZA

PAPII AKIMUANGALIA BABA YAKE ANAVYOLICHARAZA GITAA

NGUZA VICKING NA MWANAE WAKITUMBUIZA

PAPII KOCHA MTOTO WA MFALME


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...