Saturday, July 19, 2014

NDEGE NDOGO YATUA BARABARANI KWA DHARULA NCHINI UGANDA BAADA YA KUISHIWA MAFUTA


Ndege ndogo ikiwa imebeba wafanyakazi wa jeshi la Marekani imetua kwa dhalura katikati ya barabara nchini Uganda baada ya kuishiwa mafuta.
 Msemaji wa jeshi la polisi nchini Uganda, Philip Mukasa, amesema kuwa ndege hiyo iliyokua imebeba abiria wanane wakiwemo wafanyakazi wawili wa ndege hiyo iliyokuwa ikielekea Sudani ya Kusini.

Rubani wa ndege hiyo aliamua kutua katikati ya barabara baada ya kugundua hakuwa na mafuta ya kutosha, ambapo aliamua kurudi uwanja wa kimataifa wa Entebbe na kuamua kutua kwa dharura kwenye mji wa Mityana uliopo kilomita 67 (maili 41) kutoka mji mkuu wa Kampala.

Katika dharura hiyo, hakuna mtu aliyejeruhiwa, na watu wote wametoka salama.

Haikuweza kufahamika kwa haraka sababu zilizomfanya rubani hakuelekea Sudan ya Kusini na badala yake kaamua kutua katikati ya barabara baada ya ndege hiyo kuishiwa mafuta.

BARAZA LA USALAMA LAKUTANA KUHUSU UKRAINE KUFUATIA AJALI YA NDEGE


BARAZA LA USALAMA WAKATI WA DAKIKA MOJA YA UKIMYA KUWAKUMBUKA WALIOPOTEZA MAISHA YAO KWENYE AJALI YA NDEGE

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, leo limekutana kuhusu hali nchini Ukraine, kufuatia ajali ya ndege ya Malaysia hapo jana mashariki mwa Ukraine, kwenye eneo linalodhibitiwa na waasi. Taarifa kamili na Amina Hassan
(Taarifa ya Amina)
Mwanzoni mwa mkutano wa leo, Rais wa Baraza la Usalama, Richard Gasana, amewasilisha ujumbe wa rambirambi za wanachama wake kwa familia za wahanga wa ajali hiyo, na serikali za nchi zilizopoteza raia wao
GASANA
"Naomba nyote msimame na kubaki kimya kwa dakika moja, kuwakumbuka waliopoteza maisha yao"
Akizungumza kwenye mkutano huo, Msaidizi wa Katibu Mkuu kuhusu masuala ya kisiasa, Jeffrey Feltman wakati hali inaendelea kuzorota kwa kasi nchini Ukraine, inasikitisha kuwa mwanga wa matumaini ulioonekana baada ya kutangazwa mpango wa Rais Poroshenko wa amani, ukiwemo usitishaji mapigano, sasa umedidimia haraka. Kuhusu baa la ndege ya Malaysia, ambalo chanzo chake bado hakijathibitishwa, Bwana Feltman amesema
"Katibu Mkuu amesikitishwa na ripoti zinazoonekana kuwa za kuaminika kuwa kombora la kurushwa angani lilitumiwa. Katibu Mkuu analaani vikali hiki kinachoshukiwa kuwa utunguaji wa kukusudia wa ndege ya kiraia. Tukio hili la kutia hofu ni ukumbusho wa jinsi hali mashariki mwa Ukraine ilivyo mbaya mno, na jinsi inavyoathiri nchi na familia nje ya mipaka ya Ukraine."

ANGALIA PICHA ZA WATUHUMIWA 16 WANAODAIWA KUJIHUSISHA NA VITENDO VYA UGAIDI WAKIPANDISHWA KIZIMBANI NCHINI.

ASKARI WA KUTULIZA GHASIA FFU PAMOJA NA WA MAGEREZA WAKIWEKA ULINZI MKALI WAKATI WATUHUMIWA WA UGAIDI WAKIFIKISHWA MAHAKAMANI


Baadhi ya watuhumiwa wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya ugaidi  








Monday, July 14, 2014

SHAKIRA, WYCLEF WALIVYOWASINDIKIZA GERMANY KUTWAA KOMBE LA DUNIA 2014 JANA USIKU






Mshambuliaji wa German Mario Goetze (kushoto) akishangilia bao pekee aliloifungia timu yake dhidi ya Argentina, katika dakika za nyongeza fainali za Kombe la Dunia jana usiku. German ilishinda bao 1-0

TIMU ya Germany, jana usiku imeibuka mabingwa wapya wa michuano ya Kombe la Dunia 2014 'FIFA World Cup', baada ya kuifunga Argentina kwa bao 1-0, katika mchezo wa Fainali za Kombe la Dunia uliochezwa kwenye Uwanja wa Maracana jijini Rio de Janeiro.

Timu hizo zilimaliza dakika 90 bila ya kufungana na kuongezwa dakika 30 ambapo German iliweza kuibuka na ushindi wa bao 1 lililofungwa na MARIO GOETZE, katika dakika ya 22 kati ya dakika 30 za nyongeza bao lililodumu hadi kumalizika kwa dakika hizo za nyongeza.

Germana wameweza kutwaa Kombe hilo kwa mara ya nne sasa tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo ambapo kwa mara ya kwanza ililinyakuwa mnamo mwaka 1954, 1974, 1990 na hatimaye 2014.
Mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa Hispania, Carles Puyol, akipozi mbele ya Kombe la Dunia na Mwanamitindo wa Brazil, Gisela Bundchen baada ya kombe hilo kuwasili uwanjani hapo jana kabla ya kuanza kwa fainali hizo.

RAIS KIKWETE MGENI RASMI KATIKA SHEREHE ZA MIAKA 75 YA KANISA LA TAG JIJINI MBEYA.


Kutoka kushoto ni Askofu Mkuu wa TAG Dkt Barnabas Weston Mtokambali katikati ni Rais Dkt Jakaya Kikwete na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbas Kandoro , wakiwa wanaimba wimbo wa Taifa kabla ya Sherehe kuanza Rasmi.
 Askofu Mkuu wa TAG Dkt Barnabas Weston Mtokambali  akitoa salam za Shukurani kwa Mgeni Rasmi Dkt Jakaya Mrisho Kikwete pia kutoa Historia ya kanisa la TAG toka lilipoanza mpaka sasa linatimiza Miaka 75.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia maelfu ya wananchi kwenye kilele cha Sherehe za Miaka 78 ya kanisa la Tanzania Assemblies of God katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya  Julai 13, 2014
 Baadhi ya Viongozi wa Chama na Serikali wakiwa katika maadhimisho hayo 
 Charles Mwakipesile akiwatunza watoto baada ya kusoma Bibilia kwa umakini kutoka kichwani
 Sherehe zimepamba moto
 Baadhi ya Wageni waalikwa kutoka Nje ya nchi waliokuja kuhudhuria Miaka 75 ya TAG
 Ankali Issa Michuzi katika Sherehe hizo za Miaka 75 ya TAG
 Askofu Mkuu wa TAG Dkt Barnabas Weston Mtokambali katikati akiwa anazungumza jambo wakati walipokuwa wakijiandaa kutoa zawadi mbalimbali.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua kitabu cha Tanzania Assemblies of God (TAG) akiwa na Askofu Mkuu wa TAG Dkt Barnabas Weston Mtokambali wakati wa kilele cha Sherehe za Miaka 78 ya kanisa hilo katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya  Julai 13, 2014
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikabidhiwa tuzo na Askofu Mkuu wa Tanzania Assemblies of God (TAG) Dkt Barnabas Weston Mtokambali wakati wa kilele cha Sherehe za Miaka 78 ya kanisa hilo katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya leo Julai 13, 2014
 Baadhi ya wadau
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Baadhi ya Viongozi wa Kanisa la TAG kutoka Marekani 
 Watoto wakitoa Burudani 
Picha ya Pamoja baada ya Sherehe kumalizika
Picha zote na Mbeya yetu.

Wednesday, July 2, 2014

IDADI YA WATU WALIOKUFA KATIKA AJALI YA NDEGE YA MIZIGO JOMO KENYATTA LEO ALFAJIRI WAFIKIA WA



254
Askari wa Jeshi la Kenya wakiwa eneo la tukio wakijaribu kutoa msaada katika Ndege ya mizigo iliyoanguka leo asubuhi katika eneo la Utawala kwenye Uwanja wa Jomo Kenyatta, jijini Nairobi.
Taarifa kutoka Kenya zinasema kuwa mpaka sasa imefahamika kuwa jumla ya watu wanne akiwamo Rubani, waliokua kwenye ndege hiyo wameripotiwa kufa baada ya ndege hiyo kuanguka dakika chache tu baada ya kupaa kutoka kwenye uwanja huo ikielekea Moghadishu, Somalia.
Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo ambapo imeelezwa kuwa ndege hiyo ilikua iondoke mapema kusafirisha zao la Mirungi na bidhaa nyinginezo kuelekea Somalia.
Akithibitisha ajali hiyo Mkuu wa Polisi wa Jiji la Nairobi, Benson Kibue, amesema kuwa kuwa Ndege hiyo yenye nambari 5Y-CET ilianguka kwenye paa la jengo la kibiashara wakati likijaribu kutua ghafla baada ya kutokea hitilafu katika ndege hiyo na kushika moto kisha kuanza kuteketea na watu wanne waliokua ndani.
Aidha kwa mujibu wa Mkuu wa Polisi wa Jijini Nairobi, Benson Kibue, amesema kuwa katika ajali hiyo walinzi wawili walijeruhiwa mmoja ametibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani huku mmoja akilalazwa katika hospitali ya Mama Lucy.
Polisi wanaendelea na uchunguzi kwenye mabaki ya ndege hiyo kuona iwapo kuna waathirika zaidi.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...