 |
| MAREHEM HUSSEIN SEMDOE MWANDISHI WA GAZETI LA MWANANCHI ALIYEFARIKI KWENYE AJALI |
WAANDISHI wa habari wawili pamoja na Ofisa Uhamiaji wa
Wilaya ya Handeni wamefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea leo majira
ya saa nne asubuhi nje kidogo ya Mji wa Handeni. Waliofariki dunia ni Hussein
Semdoe mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Hamis Bwanga wa Radio Uhuru na
Abood pamoja na Mariam Hassan ambaye ni Ofisa Uhamiaji Wilaya ya Handeni.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu amethibitisha kutokea kwa ajali
hiyo pamoja na vifo vya marehemu hao. Mkuu huyo wa Wilaya hiyo amesema ajali hiyo imetokea wakiwa kwenye msafara
kuelekea Ndolwa kupanda miti.
Akifafanua zaidi juu ya ajali hiyo, Muhingo alisema gari lililopata ajali ni
la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Handeni, STJ 4673 ambalo ndilo lililokuwa
likitumiwa na Ofisa Uhamiaji, Hassan pamoja na wanahabari hao.
Akizungumzia mazingira ya ajali alisema ajali imetokea baada ya gari hilo
kupasuka tairi la nyuma likiwa kwenye mwendo kisha kupoteza uelekeo na
kuanguka. “Baada ya kupoteza uelekeo lili binuka kando ya barabara na marehemu
wote walitupwa nje ya gari na kuangukia mawe hivyo kupoteza maisha, wawili
walifia papo hapo na mmoja baadaye,” alisema Muhingo.
Alisema dereva pekee ndiye aliyenusurika katika ajali hiyo na amelazwa kwa
matibabu katika Hospitali ya Wilaya Handeni. “…Dereva naye alirushwa nje wakati
wa ajali pamoja na marehemu wote, lakini yeye aliangukia juu ya kichaka hivyo
kutoumia sana,” alisem kama wenzake.
Alisema msiba huo ni mkubwa kwa Wilaya ya Handeni kwani wamepoteza
wachapakazi na watu muhimu katika mchakato wa maendeleo ya wilaya hiyo.
Aliongeza kuwa Wilaya ya Handeni imepoteza wanahabari kwa asilimia 100, kwani
waandishi hao ndiyo waliokuwa wanahabari pekee wilayani hapo. “…Msiba huu ni
mkubwa si kwa tasnia ya wanahabari pekee bali hata kwa juhudi za maendeleo ya
Wilaya ya Handeni, tulikuwa tukizunguka nao katika shughuli mbalimbali hapa
Wilayani hivyo ni pigo kubwa,” alisema muhingo.
Aliongeza kwa upande wa Ofisa Uhamiaji, marehemu Hassan alikuwa ni
mpambanaji mkubwa wa wahamiaji
haramu katika wilaya Hiyo, na hivi karibuni alifanikiwa kuwakamata takribani
wahamiaji 70 eneo hilo, hivyo kifo chake ni pigo kubwa kwa nguvu kazi ya
wilaya. Alisema tayari miili ya marehemu wawili (Mdoe na Hassan) imechukuliwa
kwa shughuli za mazishi na mmoja bado (Bwanga) unasubiri wanandugu kutoka
Handeni.
(HABARI NA PICHA KWA HISANI YA THE HABARI.COM)