Friday, December 20, 2013

HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA,OKWI ATUA DAR NA KUPATA MAPOKEZI MAKUBWA

Okwi akizungumza na Waandishi wa Habari
Anatoka kuelekea kwenye gari
Anasindikizwa na Polisi
Ndani ya gari kiti cha nyuma na Katabaro
Dereva Seif Magari anaondoa gari 'mdogo mdogo' (PICHA KWA HISANI YA BIN ZUBEIR)
Mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Emmanuel Okwi amewasili jana mchana majira ya saa 9:45 katika uwanja wa ndege wa Mwalimu JK Nyererer akitokea nchini Uganda kwa shirika la ndege la Rwanda Air.


Okwi amekuja kujiunga na timu yake mpya Yanga SC ambayo ataanza kuitumikia katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya Kimataifa.
Mara baada ya kuwasili JK Nyerere Okwi alipokelewa na vipngozi wa kamati ya mashindano sambamba na washabiki, wapenzi na wadau wa soka kwa ujumla.
Okwi akiongea na waandishi wa habari uwanja wa ndege amesema anashukuru kwa kufika salama jijini Dar es Salaam na hasa katika timu yake mpya ya Yanga.
Kikubwa ameahidi kucheza kwa uwezo wake wote kuhakikisha anaisaidia timu yake mpya kufanya vizuri katika mashindano yote.
Okwi mara baada ya kuwasalimia washabiki na wanachama wa Yanga uwanja wa Kaunda moja kwa moja ameungana na wachezaji wenzake katika kambi iliyopo Protea kujiandaa na mchezo wa jumapili.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...