Sunday, March 2, 2014

ANGALIA PICHA JINSI YANGA WALIVYOKATA NGEBE ZA WAARABU

YANGA YAITANDIKA AL AHLY BAO 1 - 0 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR LEO

 Kikosi cha Yanga 
 Kikosi cha Al Ahly
 Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Mrisho Ngassa akiondoka na mpira huku Beki wa Timu ya Al Ahly ya Misri akitafuta namna ya kumzuia katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
 Kiungo mchezeshaji wa Yanga,Haroun Niyonzima akitafuta namna ya kuwatoka mabeki wa Timu ya Al Ahly ya Misri katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
 Kiungo mchezeshaji wa Yanga,Haroun Niyonzima akizuiwa na Beki wa Timu ya Al Ahly ya Misri,Ramy Abdel Aziz katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
Kipa wa timu ya Al Ahly ya Misri,Sherif Ekramy Ahmed akida moja ya hatari iliyokuwa ikielekeshwa langoni kwake na Mshambuliaji wa Yanga,Hamis Kiiza.
 Heka heka ya kuwania mpira wa Kichwa.
 Mshambuliaji Machachari wa timu ya Yanga,Emmanuel Okwi akiwachachafya mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri katika mchezo wao uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wa kuwania tiketi ya kusheza 16 bora ya Klabu Bingwa Barani Afrika.katika mchezo huo,Yanga imeifunga timu ya Al Ahly bao 1 - 0. 
 Emmanuel Okwi wa Yanga akichezewa faulo na mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri.
 Heka heka langoni mwa timu ya Al Ahly.
Mshambuliaji Emmanuel Okwi wa Yanga leo ndio alikuwa mwiba kwa timu ya Al Ahly,maana alikuwa akikabwa na Mabeki wawili wawili........
 Kipa wa timu ya Al Ahly ya Misri,Sherif Ekramy Ahmed akiruka mithili ya nyani wakati akiokoa moja ya hatari zilizokuwa zikielekezwa langoni kwake.
 Okwi anatafuta namna ya kuchia shuti.
 Mshambuliaji wa Yanga,Didier Kavumbagu akiwania mpira na Mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri.
 Ulinzi maridhawa kabisa ulitawala Uwanjani hapa.
 Ilikuwa ni nyomi la hatari.
Wachezajiwa timu ya Yanga wakishangilia ushindi wao sambamba na Mashabiki wao lukuki waliofurika uwanjani hapa.

Mfungaji wa bao pekee la Yanga,Nadir Haroub akirejea uwanjani baada ya kutoka kushangilia pamoja na washabiki wao.
 Benchi la ufundi la Al Ahly ya Misri.
 Benchi la Yanga.
 Mashabiki wa Al Ahly wakishangiliwa mwanzo mwisho,wakisaidiwa na Mashabiki wa timu ya Simba. 
 Okwiiiiiiii.......
Kocha wa Al Ahly akihaha kutoa maelekezo kwa Wachezaji wake. 
 Mabeki wa timu ya Yanga,Nadir Haroub pamoja na Kelvin Yondani wakiwa wamejipanga vyema kuuzuia mpira wa Mshambuliaji wa timu ya Al Ahly,Moussa Yedan.
 "Poa tu mwana,hii ni fea pleii tuuuuu......" 
 Ni shangwe tupu kwa Mashabiki wa timu ya Yanga uwanjani hapa hii leo. 
Mashabiki wa timu ya Al Ahly wakifungasha virago vyao baada ya kulala kwa bao 1 - 0.
 Kocha wa Yanga akisema na wachezaji wake mara baada ya kipenga cha mwisho kulia.
 Kufungwa kubaya jamaniiiiii....
 Mara baada ya Yanga kupata Goli la kwanza na la pekee,Mashabiki wa Simba walianza tena kunyoa viti na kuwarushia mashabiki wa timu ya Yanga waliokuwa wakishangilia ushindi wao huo. 
 Wazee wa feva wakiwatuliza washabiki hapo wa Simba.
Cheki mapengo ya kung'olewa kwa viti uwanjani hapa.Hali hii ni nani anatakiwa kuidhibiti???


 Wachezaji wa Yanga wakimpongeza Nahodha wao Nadir Haroub 'Canavaro', baada ya kuifungia timu yake bao pekee katika mchezo wa leo dhidi yao na Al-Ahly ya Misri uliomalizika jioni hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Canavaro amefunga bao hilo kufuatia mpira wa Kona iliyopigwa na Simon Msuva katika dakika ya 82. 
 Hongera Nahodha wetu.......
 Hili ndilo bao la Canavaro, Kipa wa Al-Ahly akiwa hoi chini baada ya kuchambuliwa......
 Kipa wa Al-Ahly akitafakari baada ya kufungwa bao hilo.....
 Mashabiki wa Yanga wakishangilia bao hilo...
 Uwanja ulijaa kama hivi......
 Mashabiki wa Simba waliokuwa wakiishangilia timu ya Al-Ahly wakiendelea na zoezi la kung'oa viti kama kawaida yao.....
 Mtanange ukiendelea uwanja wa Taifa, huku timu zote zikikosa kosa, hapa ni katika harakati za Yanga kukosa bao na Al Ahly kuokoa, mpaka sasa hakuna time yeyote iliyokwisha liona lango la mwenzake bado ni 0-0, sasa mpira ni kipindi cha pili.
 Hamis Kiiza, akijikunja kupiga shuti lililomtesa vilivyo kipa wa Al Ahly.
 Simon Msuva kijilaumu kukosa bao baada ya heka heka na jitihada alizoonyesha uwanjani katika kipindi cha kwanza.(PICHA ZOTE KWA HISANI YA MICHUZI BLOG NA SUFIANI MAPHOTO)

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...