Thursday, August 6, 2015

BREAKING NEEEEEWS. HATIMAYE PROF LIPUMBA AACHIA NGAZI RASMI NAFASI YAKE YA UENYEKITI KATIKA CHAMA CHA WANACHI CUF

Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahim Haruna Lipumba
Hatimae mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF professor Ibrahim Haruna Lipumba ametangaza rasmi kujiuzulu nafasi yake ya uenyekiti katika chama cha wanachi CUF. 

Prof Lipumba amesema ameamua kuachia nafasi hiyo na kuwa mwanachama wa kawaida kwa kuwa hakubaliani na wenyeviti wenza wa UKAWA kwa kuwakubali wanachama wa chama cha mapinduzi waingie UKAWA ikizingatiwa kuwa watu hao walishiriki katika kuipitisha katiba inayopendekezwa ambao yeye na wenzake waliipinga kwa nguvu zote.

Amesema dhamira yake imemsuta hivyo hawezi kuendelea kuwepo katika nafasi hiyo na hivyo ameamua kuwa mwanachama wa kawaida.

Prof Lipumba ametangaza azma yake hiyo katika ukumbi wa hoteli ya PEACOCK jijini Dar es Salaam na aliwasili hotelini hapo akiwa na watu wengine kabisa tofauti na ilivyokawaida kuwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho na alikuwa kavalia mavazi ya kawaida tofauti na inavyokuwa siku zote ambapo huwa anavalia mavazi ya chama hicho.

Iliripotiwa jana kuwa prof Lipumba alitaka kutangaza adhma yake hiyo jana katika ofisi za chama hicho Buguruni Dar es Salaam lakini azma hiyo ilizimwa na wazee na baadhi ya wafuasi wa chama hicho.

Tuesday, February 17, 2015

MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA 13 ASIMIKWA RASMI KUWA CHIFU WA WAHEHE

Mwanafunzi wa darasa la saba Adam Abdul Sapi Mkwawa(13) ametawazwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wahehe kufuatia kifo cha baba yake mzazi Abdul Sapi Mkwawa(66).

Rais Jakaya Kikwete alikuwa ni mmoja kati ya watu waliohudhuria maziko ya Chifu Abdul Sapi Mkwawa katika kijiji cha Kalenga mkoani Iringa na baadae kushuhudia kusimikwa kwa chifu huyo mpya wa kabila la wahehe Adam.

 Kusimikwa kwa mtoto huyo anayesoma katika shule ya msingi Highland iliyopo mkoani Iringa kutasubiri hadi atakapotimiza miaka 20 ndiyo ataanza kutumikia wadhifa huo wa uchifu ambapo kwa sasa wadhifa huo utashikiliwa kwa muda na mdogo wa marehemu Salehe hadi hapo Adam atakapotimiza umri huo(20).
Chifu mpya wa kabila la wahehe Adam Abdul Sapi Mkwawa

Rais Jakaya Kikwete akimfariji Chief Adam Abdul Sapi Mkwawa




Wazee wz kimila wakimsimika Adam Abdul Sapi Mkwawa kuwa chifu mpya wa kabila la wahehe siku mbili baada ya kifo cha baba yake Abdul Adam Sapi Mkwawa aliyekuwa chifu wa kabila hilo


RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE AONGOZA MAZISHI YA CHIFU ABDU MFWIMI ADAM MKWAWA KATIKA KIJIJI CHA KARENGA IRINGA FEBRUARI 16, 2015



5
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitia saini katika kitabu cha maomborezo baada ya kuwasili kushiriki mazishi ya aliyekuwa Chifu wa Kabila la Wahehe, Chifu Abdu Mfwimi Adam Mkwawa katika  Kijiji cha Karenga Februari 16, 2015.
7
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpa pole mjane wa aliyekuwa Chifu wa Kabila la Wahehe, Chifu Abdu Mfwimi Adam Mkwawa leo  Kijiji cha Karenga Februari 16, 2015.
3
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji  Chifu mpya wa Wahehe, Chifu Adam Abdu Mkwawa, Mtwa Adam wa Pili (14), wakati wa mazishi ya baba yake aliyekuwa Chifu wa Kabila la Wahehe, Chifu Abdu Mfwimi Adam Mkwawa  katika eneo la Nyumba ya Makumbusho ya Chifu Mkwawa, Kijiji cha Karenga  Februari 16, 2015
9dhdh
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo kaburini wakati wa mazishi ya aliyekuwa Chifu wa Kabila la Wahehe, Chifu Abdu Mfwimi Adam Mkwawa   katika eneo la Nyumba ya Makumbusho ya Chifu Mkwawa, Kijiji cha Karenga Februari 16, 2015.

Wednesday, February 11, 2015

JENGO LA GHOROFA 2 LIMETEKETEA NA MOTO JIJINI DAR

KIKOSI CHA ZIMA MOTO WAKIWA KAZINIKUJITAHIDI KUZIMA MOTO ULIOTOKEA KATIKA MAKUTANO YA BARABARA YA LIIBYA NA MSIKITI KATIKA YA JIJI



KIKOISI CHA KUZIMA MOTO WAKIWA KAZINI KUZIMA MOTO ULIOTOKEALEO


JENGO LILILOUMGUA MOTO

WAFANYAKAZI WA KIKOSI CHA ZIMAMOTO

KAMANDA SULEIMAN KOVAAKIWA KATIKAA ENEO LA TUKIO LA MOTO






Wednesday, December 31, 2014

TUSUPPORT VYA KWETU, TANZANIA INA VIPAJI!!

Tupende na tuuenzi utamaduni na asili yetu watanzania, Ak'O-Mpiruka sound band ni kikundi cha vijana wa kitanzania wenye vipaji lukuki ikiwemo kupiga na kucheza muziki wa asili, kucheza na nyoka, kucheza na moto, kujinyonga viungo, sarakasi na vingine vingi.



Ukiwa na Ak'O-Mpiruka sound ni burudani tu



Utashawishika haswa ukiwaona wanafanya mambo yao LIVE katika shughuli yoyote ile mahali popote iwe ni Harusi,Tamasha, Hotelini, Mjumuiko wa watu, Mjumuiko wa Makampuni na au Matukio Maalum




Embu tazama jinsi vijana hawa wa kitanzania wanavyotumia vizuri vipaji vyao,Bonyeza link hapo chini.

https://www.youtube.com/watch?v=YvHr-T4Es0E


Ak'O-Mpiruka sound New song ASUBUHI

http://hu.lk/rtttstvcj9q8


Tuuenzi Utanzania, Tusupport vya kwetu


www.akomungoma.co.tz

Wednesday, October 29, 2014

RAIS WA ZAMBIA MICHAEL SATA AFARIKI DUNIA



Rais wa Zambia Michael Sata amefariki dunia nchini uingereza alikokuwa anapatiwa matibabu ya ugonjwa ambao mpaka kifo chake haijawekwa wazi kuwa alikuwa anaumwa nini.

Rais Sata ambae alikuwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Mfalme Edward VII amefariki usiku wa kuamkia leo akiwa na umri wa miaka 77.

Taarifa zinasema rais huyo wa Zambia aliaga dunia baada ya mapigo ya moyo kupanda ghafla.

Hakuna taarifa ya mara moja juu ya mtu atayemrithi Rais Sata,suala hilo litaamuliwa na baraza la mawaziri la nchi hiyo linalotarajia kukutana leo Jumatano asubuhi.

akitangaza kifo cha rais huyo,katibu wa baraza la mawaziri Roland Msiska kwenye televisheni ya taifa ya nchi hiyo,alisema kwa masikitiko na mshtuko mkubwa,natangaza kifo cha rais wetu mpendwa Michael Sata.

Aliongeza kwa kusema kuwa mke wake na mtoto wake wa kiume walikuwa pembeni yake wakati rais huyo anakata roho.

Akawataka wazambia wote kuwa watulivu,wamoja kwa kipindi hiki kigumu cha msiba uliolikumba taifa hilo.

kifo cha Rais Sata kimekuja siku chache baada ya Zambia kuadhimisha miaka 50 ya uhuru kutoka kwa Waingereza.

Rais Sata anakuwa Rais wa pili wa Zambia kufariki dunia akiwa madarakani mwingine alikuwa ni Levy Mwanawasa alifariki dunia mwaka 2008.





Friday, October 24, 2014

MOTO WATEKETEZA MAGHALA 5 NA KUUNGUZA TANI ELFU TATU ZA MASHUDU MKOANI SINGIDA




Maghala matano ya kiwanda cha maunt meru Oil Miller cha mjini singida kimeteketea kwa moto na kuunguza zaidi ya tani elfutatu za mashudu ikiwemo mashine ya kukamulia mafuta na kusababisha hasara ya mamilioni ya fedha.

Akieleza mkuu wa mkoa wa singida Dk.Parseko Kone amesema   kiwanda hicho ambacho kimeanza kuungua majira ya saa tano usiku wa tarehe ishini natatu hadi sasa,imebidi mkoa kuomba gari lingine kutoka mkoa wa jirani wa manyara ili kuweza kusaidia kuzima moto ambao bado unaendelea kuwaka.
 
Kwaupande wake kamanda wa polisi mkoa wa singida  kamishina msaidizi wa jeshi la polisi Bwana Thobias Sedoyeka amethibitisha kuungua kwa kiwanda hicho na  jeshi la polisi limejitahidi kuweka ulinzi  na  amewataka wananchi kutoa taarifa mapema pindi matukio kama hayo yanapo tokea.
 
Meneja wa kiwanda hicho Bwana Sajay Sumarzya  amesema wao walipata taarifa kutoka kwa walinzi usiku majira ya saa tano  na walipo fika walikuta maghala matano ya mashudu  yenye tani zaidi ya elfutatu  yakiwaka moto.

MUONEKANO WA KITUO KIPYA CHA DALA DALA KILICHOHAMISHWA KUTOKA UBUNGO


GAR LA DALADALA LIKITOKA KATIKA KITUO KIPYA CHA DALADALA CHA MAWASILIANO

BAADHI YA MAGARI YA DALADALA
 KATIKA KITUO KIPYA KINACHOJULIKANA KAMA SINZA TEMINAL ENEO LA MAWASILIANO

ABIRIA WAKIWA KATIKA KITUO KIPYA CHA DALADALA


MAGARI YAKICHEKIWA

HATA UDA YUPO KATIKA KITUO HICHO

BAADHI YA ABIRIA WAKIHANGAIKA KUTAFUTA KIBAO KINACHOANDIKWA SEHEMU ANAYOKWENDA(PICHA NA  MZUKA WA FUNGO)

WANANCHI WA MKOA WA KILIMANJARO WAONDOLEWA HOFU YA KUWEPO MGONJWA WA EBOLA MKOANI HUMO

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama
Uongozi wa mkoa wa kilimanjaro umewaondoa hofu wananchi wake juu ya ugonjwa hatari wa Ebola kutokana na kuwepo mgonjwa anayehudumiwa katika zahanati ya Shirimatunda katika manispaa ya Moshi aliyedhaniwa kuwa na dalili za ugonjwa huo.

Mkuu wa mkoa huo bwana Leonidas Gama amewataka wananchi hao kuondoa hofu hiyo kwa kuwa mgonjwa huyo mwanaume amethibitika kuwa ana Maleria kali ambayo imekuwa ikimsumbua.

Awali kulikuwa na taarifa kuwa Halmashauri ya manispaa ya Moshi imeifunga zahanati ya kata ya Shirimatunda na kuwahamisha wagonjwa wanaouhudumiwa na zahanati hiyo katika Hospitali za manispaa hiyo ikiwemo ya Mtakatifu Joseph kwa hofu ya kuwepo kwa mgonjwa anayehudumiwa kwenye zahanati hiyo anadhaniwa kuwa na ugonjwa wa Ebola.

Wednesday, October 22, 2014

MIAKA 10 TANGU KIFO CHA FREDY NDALA KASHEBA

ndala-kasheba_2255445 
LEO tunatimiza miaka kumi toka kifo cha mwanamuziki mahiri Freddy Supreme au maarufu kama Ndala Kasheba. Freddy alianza kufundishwa gitaa na baba yake wakati akiwa na umri wa miaka 12. Baba yake alijua kupiga gitaa japo hakufanya kazi ya uanamuziki, alikuwa akipiga gitaa nyumbani baada ya saa za kazi. Moja ya bendi maarufu ambazo zilimtambulisha sana Fredd ilikuwa Orchestra Fauvette, Freddy alieleza kuwa bendi ya Orchestra Fauvette ilianza tarehe 7 mwezi wa sita mwaka 1964 katika jiji la Lubumbashi huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. Jina hilo Fauvette kwa kiswahili ni Chiriku, bendi ilikuwa na muimbaji ambaye waliamini alikuwa anaimba kama chiriku na hivyo kuipa bendi hiyo jina hilo. Vyombo vyao vya muziki walinunua Ujerumani kupitia duka la muziki la Dar es salaam Music House (duka lipo mpaka leo). Vyombo vilikuwa  vya aina ya Hofner, jina lililoheshimika sana kwa wanamuziki wakati huo.
IMG_2110
HILI NDILO KABURI LA FREDY NDALA KASHEBA LILIPO KINONDONI JIJINI DAR

Kati ya nyimbo ambazo zilipigwa katika kipindi hicho ni Camarade ya nzela, ambayo Freddy alieleza ni wimbo uliokuwa ukizungumzia rafiki wa kukutana nae barabarani au njiani, ambaye roho yake huwa kama sanduku la nguo, ambalo ndani yake huwezi kujua kuna nini. Pia ulipigwa wimbo Jacqueline ambao ulitungwa na mwenyewe Freddy ambao alieleza alikuwa alimtungia mpenzi wake aliyempenda Jacqueline. Wimbo mwingine uliopigwa katika kipindi hicho ni Nono na Kalemie, wimbo huu ulitunguiwa binti aliyeitwa Nono mkazi wa Kalemie ambaye alikuwa mpenzi mkubwa wa bendi ya Fauvette.
  Fauvette ilifika Dar na kuwa inapiga katika ukumbi wa White House Ubungo, lakini kwa miaka hiyo Ubungo ilikuwa mbali sana na mji, na kulikuwa na ajali nyingi zikiwapata wapenzi wa bendi katika usafiri wa kutoka kwenye muziki, hivyo bendi ikaamua kuhamia ukumbi wa Mikumi Tours ambapo walikuwa wakipiga Ijumaa, Jumamosi na Jumapili. Fauvette walikuwa na ndoto ya kuwa bendi bora Afrika. Hawakufikia huko lakini waliweza kuweka alama kubwa katika historia ya muziki wa Afrika mashariki na Kati
Kasheba aliweza kuimarisha jina lake zaidi alipolifanya maarufu gitaa la nyuzi kumi na mbili, mwenyewe akiliita nyuzi dazani, hasa alipoanza kulipiga kwa mtindo wa Dukuduku akiwa Safari Sound Orchestra. Pamoja na bendi hizo Kasheba pia alipitia Safari Nkoy, Zaita Muzika, Kasheba group, pia alipita Maquis, na kwa wiki chache alipitia Tancut Almasi.

Kasheba alifariki 22 Oktoba 2004 akiwa na miaka 58.

Tuesday, October 21, 2014

OSCAR PISTORIUS AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MITANO JELA


Oscar Pistorius amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela baada ya kukutwa na hatia ya kuua bila kukusudia kwa kumpiga risasi aliyekuwa mpenzi wake Reeva Steenkamp mwezi wa pili mwaka jana.Pia amehukumiwa miaka mitatu kwa kosa la kutumia vibaya silaha aliyokuwa anaimiliki kisheria lakini hukumu hiyo imesimamisha na badala yake atatumikia miaka mitano yote kwa pamoja.
oscar 2 oct 21 
Hukumu hiyo imetolewa na jaji mwanamama Thokozile Masipa baada ya kusikiliza kwa makini na kupima hoja za kila upande dhidi ya kesi hiyo iliyokuwa inamkabili mwanariadha huyo wa Afrika kusini.


Pia hukumu ya miaka mitatu imetolewa baada ya kuitumia bastola kinyume na sheria pale alivyoifyatua chini ya meza kwenye mgahawa wa Tasha uliopo Johannesburg mwezi January mwaka 2013,mwezi mmoja kabla hajamuua mpenzi wake siku ya wapendanao february 14,2013.

HUKUMU ILIVYOSOMWA

Katika hukumu yake,jaji Masipa alianza kusoma mwenendo mzima wa kesi jinsi ilivyokuwa inaendeshwa na hoja mbali mbali kutoka upande wa mashtaka na upande wa utetezi katika mahakama kuu mjini pretoria Afrika kusini.

Pistorius amepatikana na hatia ya kuua bila ya kukusudia mwezi uliopita baada ya kusababisha kifo cha Reeva Steenkamp pia kutumia sdilaha kinyume cha sheria tukio ambalo alilifanya kwa nyakati tofauti na lile la mauaji.

Jaji Masipa alisema wakati wa kuendesha mwenendo mzima wa kesi hiyo alikuwa na washauri wawili waliokuwa wanamsaidia katika kupima kila hoja zilizokuwa zinatolewa na pande mbili,lakini uamuzi wa hukumu ni wakwake yeye binafsi.

Alisema wakati mwingine kupata hukumu stahiki ni vigumu sana tatizo ambalo linazikabili mahakama nyingi zinazoendesha makosa ya jinai.


Masipa amesema kabla ya hukumu,upande wa utetezi ulipeleka mashahidi wanne wakatoi upande wa mashtaka uliita wawili tu katika kuthibitisha mashtaka waliyoyawasilisha mbele ya mahakama.

Akielezea ushuhuda wa daktari wa saikolojia Dr Löre Hartzenberg alisema kuwa alikuwa akimtibu Pistorius tangu alipofanya mauaji hayo mwezi february mwaka jana.
.

Hartzenberg alisema mahakama haina budi kuzingatia maisha ambayo amekuwa nayo mara baada ya tukio,kwani alipoteza marafiki,hakuweza kuendelea na kazi yake,na alikuwa ameathirika kisaikolojia.

Masipa alisema shahidi wa pili  Joel Maringa, ambae ni afisa ustawi wa jamii alipendekeza Pistorius angekuwa kwenye kifungo cha ndani lakini nyumbani kwake kwa miaka mitatu na kufanya kazi za kijamii kwa masaa yasiyopungua 16 kwa mwezi.

Meneja wa Pistorius Peet van Zyl, alikuwa ni shahidi wa tatu aligusua kuhusu matembezi ya hisani aliyopanga kuyafanya kuhusu kazi aliyokuwa anaifanya.

Ushahidi wa Van Zyl ulisema kwamba kabla hajamuua mpenzi wake kwa risasi,Pistorius alikuwa anaheshimika kama mwanamichezo mahiri ulimwenguni,amabae alitumia muda na pesa zake katika mambo mengi ya msingi.

Kwa mujibu wa  Van Zyl, amesema fursa ya pistorius kushiriki kwenye mambo yote hayo imesimamishwa tangu kifo Steenkamp

Shahidi wa nne ambae pia ni afisa ustawi wa jamii Annette Vergeer, ambae alitumia muda mwingi kuelezea hali mbaya na tete ya magereza ilivyo nchini humo.

Ameiambia mahakama kuwa jela za nchini humu hazikidhi mahitaji maalum ya Pistorius kulingana na hali yake.

Kwa upande wa mashahidi wa mashtaka dhidi ya Pistorius wa kwanza alikuwa ni binamu yake marehemu Steenkamp Kim Martin,ambae alielezea kwa undani kazi za mwanamitindo huyo marehemu pamoja na maisha yake binafsi yalivyokuwa.


Martin aliiambia mahakama jinsi Steenkamp alivyokuwa karibu saana na wazazi wake,Barry na June na aliwasaidia sana kifedha na walikuwa wakimtegemea kwa kila kitu.Jaji Masipa alibaini jinsi gani Martin alivyokutana na Pistorius kwa mara ya kwanza mwezi mmoja kabla ya kifo cha Steenkamp.Martin alikumbusha mahakama kuhusu taharuki iliyoikumba familia yao baada ya kupata taarifa ya kifo cha ndugu yao.

Alisema hali ya afya ya baba mzazi wa Steenkamp, Barry ilikuwa mbaya kwani alikuwa na msongo wa mawazo baada ya kifo cha mwanae.

Shahidi wa mwisho kwa upande wa mashtaka alikuwa ni kaimu mkurudenzi wa taifa idara huduma urekebishaji tabia Zac Modise alisema mfumo wa jela za nchi hiyo ni mzuri na unaweza kumhifadhi Pistorius.


Jaji Masipa aligusia namna upande wa utetezi ulivyotoa hoja kuwa Pistorius asiende jela kwa kuwa anahitaji msaada wa matibabau ya kisaikolojia na akakubaliana na hoja ya shahidi wa mashitaka bwana Modes kuwa huduma za aina hiyo zinapatikana na mwanariadha huyo anaruhusiwa kumpeleka daktari wake huko jela akamtibie.

alisema hata wanawake wajawazito ni kundi ambalo lina mazingira magumu sana kwenye jamii,na walikuwa wanakwenda jela na idara za amgereza ziliweza kuwahudumia vyema,hivyo haitakuwa vyema kwa sheria iwatazame kwa umuhimu wa kipekee watu wenye pesa na maarufu huku upande mwingine wa watu masikini waachwe.

Masipa anaamini kwamba upande wa utetezi umeegemea sana katika hoja zake kuhusu hali ya ulemavu aliyokuwa nayo Pistorius,lakini akasema ukiyaangalia maisha ya Pistorius hasa ya kazi yake alikuwa anashindana pia na watu wazima na alikuwa anashinda.

alisema hukumu yake imepangwa kuonyesha hali halisi ya Pistorius,kuwa aliweza kubadili mtazamo hasi wa watu dhidi ya ulemavu ana aliwavutia wengi hasa vijana,amesema jambo hili halitapuuzwa kamwe litaheshimiwa na kubaki kuwa hivyo japo meneja wake alisema akifungwa haya mambo yote aliyokuwa anafanya kwenye jamaii yatasimama.

Masipa anaamini  Pistorius anajutia kwa kile alichokifanya kutokana na ushahidi kwamba  alijaribu kuwatafuta wanafamilia wa Steenkamp kwa siri na kuwaomba radhi.


Baadae alimuamrisha Pistorius kusimama kisha akamhukumu miaka mitano jela kwa kuua bila kukusudia na miaka mitatu kwa kosa la pili ila ataitumikia yote kwa pamoja na miaka miwili inaanza sasa akiwa jela.

Pistorius baada ya hukumu aliweza kuwapa mikono baadhi ya wanafamilia wake kabla ya kupanda karandinga kwenda jela.


Monday, September 22, 2014

JOSE MOURINHO ADAI MAPENZI YA FRANK LAMPARD KWA CHELSEA YAMEKWISHA!


Jose Mourinho says Frank Lampard's love story with Chelsea ended when he joined a title competitor
 
Lampard slots home from inside the penalty area to send the City fans into ecstasy against his former employers
Lampard akiteleza katika eneo la penalti na kuifungia City bao.

Jose Mourinho anasema mapenzi ya Frank Lampard kwa Chelsea yalikwisha baada ya kujiunga na washindani wake

JOSE  Mourinho amesema mapenzi ya Frank Lampard kwa Chelsea yamekwisha baada ya jana kuifungia Manchester City bao la kusawazisha katika dakika za majeruhi uwanja wa Etihad.
 
Nyota huyo mwenye rekodi ya kufunga mabao mengi kwa muda wote Chelsea, alitokea benchi na kuiadhibu timu yake hiyo ya zamani, lakini Mourinho aligoma kukubali kuwa mchezaji huyo anayecheza kwa mkopo Man City ana mapenzi ya kweli kwa Chelsea.
 
Alisema: "Frank ni mchezaji wa Man City, siamini hadidhi zake na mapenzi ya moyoni kwake, labda mimi ni mshamba wa mpira"
"Alipoamua kwenda kwa washindani wa moja kwa moja na Chelsea, mapenzi kwa timu yalikwisha. Alifanya kazi yake kiuweledi.
 
"Alipokelewa vizuri England na hii ndio England na hii ndio Chelsea. Watu wa Chelsea kamwe hawasahau kile watu wa Chelsea walifanya".
 
"Iliwahi kunitokea hata mimi  nikiwa kocha wa Inter. Ni utamaduni na uzuri wa Chelsea".

CHADEMA IRINGA YATANGAZA MAANDAMANO YA AMANI JUMATATU, POLISI WAYAPIGA MARUFUKU


Frank Nyalusi Mwenyekiti wa Chadema Iringa Mjini
Kama kawaida salamu za chama hicho za Peopleziii zilisika
Mlemavu huyo aliuliza swali katika mkutano huo akitaka kujua kati ya Samwel Sitta na Rais jakaya Kikwete ni nani ana madaraka makubwa zaidi kuhusu mchakato wa Katiba
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Iringa Mjini, kimetangaza kufanya maandamano ya amani LEO Jumatatu ikiwa ni hatua ya kuitikia wito wa mwenyekiti wao, Freeman Mbowe wa kufanya maandamano hayo nchi nzima kushinikiza kusitishwa kwa Bunge la Katiba.

Mwenyekiti wa Chadema wa Iringa Mjin, Frank Nyalusi alitoa tangazo hilo jana katika mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika katika mtaa wenye machinga wengi maarufu kama Magari Mabovu, Kitanzani.

Katika mkutano huo uliohudhuriwa na vijana kadhaa huku ukiwa umezungukwa na askari Polisi kila kona, Nyalusi alisema “wapende wasipende, kesho tutafanya maandamano, tunaomba Polisi washiriki kulinda usalama wetu, kwani maandamano hayo yatakuwa ya amani.”

Alisema maandamano hayo yanalenga kupeleka ujumbe wa kusitishwa kwa mchakato wa bunge hilo kwa kuwa hauna maridhiano na fedha zitakazonusurika zitumike katika shughuli zingine za kijamii.

“Hatuwezi kupata Katiba kwa staili hiyo, tumemuomba Rais asitishe mchakato huo lakini tumepuuzwa na sasa tunadhani ni zamu ya watanzania wote kupaza sauti zao ili bunge hilo lisitishwe,” alisema.

Alipoulizwa baadaye maandamano hayo yataanzia wapi, Nyalusi hakuwa tayari kutaja ni eneo gani yataanzia kwa kile alichosema hawataki wapinzani wao wajue.

Kabla ya kutangazwa kwa maandamano hayo ya kesho jumatatu, jeshi la Polisi liliripotiwa na chama hicho kuwazuia kufanya maandamano kama hayo Jumamosi iliyopita.

Badala yake kwa mujibu wa Nyalusi, jeshi hilo liliwaruhusu kufanya mkutano wa hadhara katika eneo hilo la Magari Mabovu.

Katika mahojiano na gazeti hili, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alisema jeshi lake halijapokea maombi ya maandamano hayo kutoka katika chama hicho.

 Aliwataka wafuasi wa chama hicho kuzingatia sheria, taratibu na kanuni wakati kikipanga na kufanya mambo yake.

Akitoa ufafanuzi huo kwa njia ya simu, Mungi alisema; “nchi hii kama zilivyo nchi nyingine inaendeshwa kwa sheria. Kwahiyo watu binafsi, serikali, vyama vya siasa na wengine wote ni lazima wazingatie hilo.”

Alisema mji wa Iringa upo shwari na kwamba jeshi hilo limejipanga kikamilifu kukabiliana na hali yoyote ile itakayoonekana inataka kuhatarisha amani.
 
CREDIT:FRANCIS GODWIN

MANCHESTER CITY YATOSHANA NGUVU NA CHELSEA


IMG_7407.JPG
Baada ya Man United kupokea kipigo kutoka kwa Leicester City, miamba mingine ya ligi kuu ya Uingereza Chelsea ilijitupa uwanjani kucheza na Manchester City.
Mchezo huo uliopigwa kwenye uwanja wa Etihad umeisha kwa matokeo ya sare 1-1.Dakika chache baada ya Pablo Zabaleta kutolewa kwa kadi nyekundu Chelsea walipata goli la kwanza kupitia mchezaji aliyetokea benchi Andry Schurrle.
Akitokea benchi mchezaji wa zamani wa Chelsea Frank Lampard aliunganisha krosi ya James Milner na kuisawazishia Man City.
Mpaka mpira unamalizika Man City 1-1 Chelsea.

VAN GAAL AKUBALI KUPOTEZA MECHI

VAN GAAL

Louis van Gaal amesema timu yake ya  Manchester United imepoteza pointi tatu muhimu baada ya kuchapwa mabao 5-3 na Leicester City.

Manchester ilianza kwa kuwa mbele kwa mabao mawili lakini cha ajabu mabao hayo yalirudishwa na kuongezwa mengine katika kipindi cha pili na kuiacha Manchester United ikiendelea kupata uhaba wa ushindi.

“Van Gaal amesema huezi kuamini kuwa unaongoza kwa mabao 3-1 na upo mbele kwa goli mbili zaidi katika kipindi cha kwanza,tulitakiwa kumaliza mchezo kwa ushindi lakini tulishindwa kufanya hivyo,tulitengeneza nafasi nzuri na tukashinda magoli  mazuri lakini hayakudumu kwa dakika zote 90 tulizocheza uwanjani",amesema Van Gaal.

Mchezo ulianza kuwageukia Manchester United pale muamuzi wa mchezo Mark Clarrenburg alipowapa penati baada ya Reafael kumfanyia madhambi Jamie Vardy katika eneo la penati ambayo Van Gaal alikataa kusema chochote kuhusu maamuzi hayo ya mwamuzi.

"wakati matokeo yanasomeka 3-2 hakukuwa na tatizo,tulidhani tutaumaliza mchezo kwa ushindi,tutautawala mchezo wote ambao tuliutawala katika dakika zote kumi za mwanzo na kufunga mabao maridadi,lakini hatukuwa makini tukaupoteza mchezo" alisema Van Gaal.

Hadi mwamuzi Mark Clarrenburg anapuliza kipyenga cha mwisho,Manchester United ilikuwa imelala kwa mabao 5-3.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...