Monday, September 22, 2014

JOSE MOURINHO ADAI MAPENZI YA FRANK LAMPARD KWA CHELSEA YAMEKWISHA!


Jose Mourinho says Frank Lampard's love story with Chelsea ended when he joined a title competitor
 
Lampard slots home from inside the penalty area to send the City fans into ecstasy against his former employers
Lampard akiteleza katika eneo la penalti na kuifungia City bao.

Jose Mourinho anasema mapenzi ya Frank Lampard kwa Chelsea yalikwisha baada ya kujiunga na washindani wake

JOSE  Mourinho amesema mapenzi ya Frank Lampard kwa Chelsea yamekwisha baada ya jana kuifungia Manchester City bao la kusawazisha katika dakika za majeruhi uwanja wa Etihad.
 
Nyota huyo mwenye rekodi ya kufunga mabao mengi kwa muda wote Chelsea, alitokea benchi na kuiadhibu timu yake hiyo ya zamani, lakini Mourinho aligoma kukubali kuwa mchezaji huyo anayecheza kwa mkopo Man City ana mapenzi ya kweli kwa Chelsea.
 
Alisema: "Frank ni mchezaji wa Man City, siamini hadidhi zake na mapenzi ya moyoni kwake, labda mimi ni mshamba wa mpira"
"Alipoamua kwenda kwa washindani wa moja kwa moja na Chelsea, mapenzi kwa timu yalikwisha. Alifanya kazi yake kiuweledi.
 
"Alipokelewa vizuri England na hii ndio England na hii ndio Chelsea. Watu wa Chelsea kamwe hawasahau kile watu wa Chelsea walifanya".
 
"Iliwahi kunitokea hata mimi  nikiwa kocha wa Inter. Ni utamaduni na uzuri wa Chelsea".

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...