Friday, October 24, 2014

MOTO WATEKETEZA MAGHALA 5 NA KUUNGUZA TANI ELFU TATU ZA MASHUDU MKOANI SINGIDA




Maghala matano ya kiwanda cha maunt meru Oil Miller cha mjini singida kimeteketea kwa moto na kuunguza zaidi ya tani elfutatu za mashudu ikiwemo mashine ya kukamulia mafuta na kusababisha hasara ya mamilioni ya fedha.

Akieleza mkuu wa mkoa wa singida Dk.Parseko Kone amesema   kiwanda hicho ambacho kimeanza kuungua majira ya saa tano usiku wa tarehe ishini natatu hadi sasa,imebidi mkoa kuomba gari lingine kutoka mkoa wa jirani wa manyara ili kuweza kusaidia kuzima moto ambao bado unaendelea kuwaka.
 
Kwaupande wake kamanda wa polisi mkoa wa singida  kamishina msaidizi wa jeshi la polisi Bwana Thobias Sedoyeka amethibitisha kuungua kwa kiwanda hicho na  jeshi la polisi limejitahidi kuweka ulinzi  na  amewataka wananchi kutoa taarifa mapema pindi matukio kama hayo yanapo tokea.
 
Meneja wa kiwanda hicho Bwana Sajay Sumarzya  amesema wao walipata taarifa kutoka kwa walinzi usiku majira ya saa tano  na walipo fika walikuta maghala matano ya mashudu  yenye tani zaidi ya elfutatu  yakiwaka moto.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...