Wednesday, January 1, 2014

WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI DR WILLIAM MGIMWA AFARIKI DUNIA NCHINI AFRIKA KUSINI

ALIYEKUWA WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI MAREHEM DR WILLIAM MGIMWA

SIKU ALIYOKUWA ANAWASILISHA BAJETI YA SERIKALI YA MWAKA 2012/2013
Waziri wa Fedha, Dk. William Augustao Mgimwa (63) amefariki dunia.
 
Taarifa za hivi punde zinasema Waziri huyo wa fedha katika serikali ya awamu ya nne ya Rais Jakaya Kikwete amefariki dunia hii leo baada ya kuugua na kulazwa nchini Afrika Kusini.
Mgimwa aliyezaliowa January 20, 1950 na kuwa mbunge wa jimbo la Kalenga mkoani Iringa kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Binafsi ya Milpark ya nchini humo.
 
Dk. Mgimwa alikuwa mkufunzi katika Chuo cha Benki mkoani Mwanza, kabla ya kufanikiwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Kalenga, Mkoa wa Iringa, katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...