Monday, March 10, 2014

WATAALAMU WA USALAMA WA ANGA WATOA SABABU ZINAZOHISIWA ZIMESABABISHA NDEGE YA SHIRILA LA NDEGE LA MALAYSIA KUANGUKA



NDEGE YA SHIRIKA LA NDEGE LA MALAYSIA BOING 777 ILIYOPOTEA NA MPAKA SASA HAIJULIKANI ILIPO IKIWA NA ABIRIA ZAIDI YA 200


WATAALAM WA VIETNAM WAKIWA KATIKA NDEGE KUFUATILIA ENEO AMBALO WANAHISI NDEGE HIYO ILIANGUKA

SEHEMU HII INAONYESHA MAFUTA YAKIWA YANAELEA WATAALAM WA VIETNAM WANAHISI IMEANGUKIA HAPA
SEHEMU INAPOHISIWA KUWA NDEGE YA MALAYSIA IMEANGUKA

WAPENZI HAWA WALIKUWEMO KATIKA NDEGE HIYO NA INAHOFIWA WAMEPOTEZA MAISHA

MOJA YA FAMILIA YA WATU WALIOSAFIRI NA NDEGE HIYO

NDUGU WA ABIRIA AKILIA KWA UCHUNGU MARA BAADA YA KUPOKEA TAARIFA YA KUPOTEA KWA NDEGE HIYO

WAZAZI HAWA MAMA MWENYE SURUALI NYEUSI NA BABA MWENYE JAKETI JEUSI WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA KIJANA WAO NA MPENZI WAKE KABLA YA KUONDOKA KUALA LUMPUR NA NDEGE ILIYOPOTEA

 Wataalam wa masuala ya anga wanasema wakati mgumu na tete kwa ndege yeyote ni wakati inataka kuruka au kutua,mara chache sana matukio yasiyokuwa ya kawaida huwa yanatokea pale ndege inapokuwa angani umbali wa takribani mile saba sawa na kilometa 11 kutoka usawa wa ardhi.
  

Kwa  hiyo kwa kupotea kwa ndege ya shirika la ndege la Malaysi awakati ikiwa angani siku ya Jumamosi asubuhi ikiwa na abiria zaidi ya 200 katika bahari ya kaskazini mwa China,imefanya wataalamu wa masuala ya anga kubaini kwamba chochote ambacho kitakuwa kimetokea basi kitakuwa kimetokea ghafla na kwa haraka mno kiasi cha kumfanya hata rubani wa ndege hiyo kushindwa kupiga simu ya dharula. 


Inaweza ikachukua miezi au hata mwaka kwa wachunguzi wa ajali za ndege kubaini kile kilichotokea kwa ndege hiyo ya shirika la ndege la Malaysia boing 777 iliyoruka kutoka mji mkuu wa Malaysia Kuala Lumpur kuelekea China.


Mmoja kati ya wachunguzi hao wa ajali za ndege bw Todd Curtis ambae ni mhandisi wa masuala ya ndege mstaafu,amesema katika hatua ya awali kabisa ya uchunguzi wao wanajitahidi kutafuta ukweli wa mambo ambayo mpaka sasa hawayajui.Todd ameshafanya kazi kwenye ndege hiyo boing 777 na sasa ni mkurugenzi wa taasisi moja ya usalama wa ndege huko Malaysia Airsafe.com foundation.


Radar ya jeshi imebashiri kwamba ndege hiyo iliyopotea Boing 777 inaweza kuwa iligeuza safari iliyokuwa imeianza kabla ya kupotea,Mkuu wa shirika la ndege la Malaysia amesema siku ya Jumapili kwamba mamlaka inachunguza abiria wanne ambao utambulisho wao unamashaka.Hii itaonyesha mazingira yalivyokuwa katika dakika za mwisho kabla ndege haijapata ajali.Mkuu wa shirika la ndege hakubainisha muelekeo wa ndege hiyo kabla ya ndege hiyo kupoteza uelekeo au ilikwenda umbali gani kabla ya kupotea ila baadhi ya taarifa zinatafutwa kwa kushirikiana na radar ya mtu binafsi.


Kama zikipatikana taarifa sahihi kuwa ndege hiyo iligeuza na kurudi ilikotoka kabla ya kupotea,basi kuna uwezekano mkubwa kuwa ndege hiyo ilikubwa na tatizo kubwa wakati ikiwa angani lakini maswali mengi yanaibuka kwa nini rubani hakutoa ishara yeyote katika chumba cha kuongozea ndege ili apate msaada.Kama kulikuwa na matatizo kidogo ya kiufundi au engine zote mbili za ndege zilizima,rubani lazima angekuwa na muda wa kupiga radio ya upepo,Kutokupiga kwake radio ya upepo kunatoa picha kwamba kuna kitu cha ghafla mno kilitokea hadi akashindwa kufanya chochote, alisema William Waldock ambae anafundisha masuala ya uchunguzi wa ajali za ndege katika chuo cha Embry-Riddle Aeronautical Arizona.


Inawezekana kuwa aidha lilitokea tatizo la ghafla au kitu cha haraka kilichosababisha ikaanguka.Baadhi ya wataalam wanadhani inawezekana pia likawa ni tukio la ugaidi au rubani akawa ameiangusha kwa makusudi.





Haijalishi tukio hili limetokea kwa namna gani,lakini ni mapema mno kusema kitu halisi kilichotokea,Kitu cha msingi ni kusubiri mabaki ya ndege hiyo yatakapopatikana na kupatikana kwa kisanduku kinachohifadhi sauti na uchunguzi wa tatizo.Wachunguzi wa kimarekani kutoka FBI,Bodi ya usafiri Salama ya taifa na shirikisho la uongozi wa anga, na wataalam wa ndege aina ya Boeing wote wameelekea Asia kusaidia uchunguzi huo.

Utafutaji wa hali ya juu umeshafanyika baharini lakini mpaka sasa hakuna taarifa yeyote iliyothibitishwa kupatikana kwa ndege hiyo,ingawa Serikali huko Vietnam imesema kuwa Jumapili jioni ndege yao ilikuwa inapita chini chini katika bahari iliona kitu kama cha pembe tatu kilomita karibu 90 sawa na mile 56 kusini mwa kisiwa cha Tho Chu,sehemu hiyo hiyo ambayo mafuta yameonekana yakielea siku ya Jumapili,lakini gazeti la serikali limesema mkuu wa jeshi msaidizi wa Vietnam amekaririwa akisema kitu hicho kilichoonekana baharini ni mlango wa ndege.




Baadhi ya mambo yanayohisiwa kuwa yamesababisha ndege hiyo kupotea ni  muundo wa umbo la ndege ambao ni Alluminium,hali mbaya ya hewa,Rubani kutotambua tatizo mapema,kuzima au kushindwa kufanya kazi kwa ingini zote mbili za ndege,kupigwa bomu au kutekwa hizi ni baadhi ya sababu zinazohisiwa na wataalamu wa ajali za ndege na usalama wa anga kuwa zimesanbabisha ndege hiyo kupotea.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...