Saturday, March 16, 2013

ASILIMIA 28 YA WANAFUNZI WA KIKE AFRICA KUSINI WANA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI


Takribani asilimia 28 ya wanafunzi wa kike nchini Afrika Kusini wanaishi na virusi vya UKIMWI idadi ambayo ni kubwa ukilinganisha na asilimia 4 ya wanafunzi wa kiume wanaoishi na virusi hivyo. Waziri wa afya wa nchi hiyo Aaron Motsoaledi amesema wasichana wengi wamekuwa wakiambukizwa kutokana na kushiriki ngono na wanaume wenye umri mkubwa.
Waziri wa afya wa Afrika kusini Aaron Motsoaledi

Akitoa takwimu hizo Motsoaledi amesema wanafunzi wa kike wapatao 94,000 nchini humo wamepata ujauzito katika kipindi cha mwaka 2011, baadhi yao wakiwa katika umri wa miaka kumi.

Motsoaledi ametoa wito kwa watoto wote wa kike kutojihusisha kimapenzi na wanaume wenye umri mkubwa na kujiepusha na ngono ili kupunguza na kasi ya maambukizi ya UKIMWI miongoni mwao.

Taifa hilo lina jumla ya watu milioni 50, na takwimu za wizara ya afya zinaonyesha watu milioni 6 nchini humo wanaishi na virusi vya UKIMWI.

Afrika Kusini ni miongoni mwa nchi zenye maambukizi makubwa ya UKIMWI duniani, hata hivyo idadi ya vifo vitokanavyo na ugonjwa huo imekuwa ikipungua siku hadi siku.

Hivi karibuni idara ya afya nchini humo imeanzisha jitihada za kukabiliana na maambukizi ya VVU kwa watoto wa shule. Miongoni mwa jitihada hizo ni pamoja na upimaji wa afya kwa hiari na ugawaji wa mipira ya kufanyia mapenzi condom

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...