Friday, March 8, 2013

MFAHAM MARK ELLIOT ZUCKERBERG MTALAAM WA COMPUTER AMBAE KUPITIA UBUNIFU WAKE AMEWEZA KUWAUNGANISHA WATU BILLIONI MOJA DUNIANI KUPITIA MTANDAO WAKE WA FACEBOOK

MARK ZUCKERBERG FACEBOOK CEO




MARK AKIWA NA MKEWE PRISCILLA


RANDI


Randi Zuckerberg dada yake mark ambaye ni mmoja wa maofisa wa juu wa facebook Inc






Mark Elliot Zuckerberg alizaliwa May 14,1984,ni mtaalam wa programmes za computer na mjasiliamali wa masuala ya tovuti wa kimarekani,anajulikana zaidi kama miongoni mwa watu watano waasisi wa mtandao wa kijamii,facebook. Zuckerberg ni mwenyekiti na mtendaji mkuu wa kampuni ya mtandao wa kijamii Facebook inc na utajiri wake ambao umetokana na mtandao huu wa kijamii facebook unakadiriwa kuwa dola za kimarekani bilioni 9.4,na mahesabu haya ni kwa mwaka 2012.

Zuckerberg alizaliwa na kukulia  New York Marekani, alianza kujishughulisha na mambo ya computer akiwa middle school kama hobby tu, kwa msaada wa baba yake na mwalimu wake aliyependa kumwita Zuckerberg jina la prodigy. Akiwa high school  Phillips Exeter Academy alipendelea sana fasihi katika lugha.
 
Baadae akajiunga na Havard College hapo akachukuwa masomo ya computer science na saikolojia.Akiwa chuoni hapo aliwahi kubuni mtandao aliouita FACEMASH, ambao uliwawezesha wanafunzi kupitia mtandao wa chuo kupiga kura.Kutokana na kubuni mtandao huu kupitia mtandao wa chuo,ulisababisha mtandao huu ufungwe na akachukuliwa hatua za kinidhamu.

Pamoja na wanafunzi aliokuwa anakaa nao katika chumba kimoja na baadhi ya aliokuwa nao katika chuo kikuu cha Havard ambao ni Eduardo Saverin, Andrew Mc Collum, Dustin Moskovitz na Chris Hughes wakaizindua Facebook katika chumba cha bweni lao.Baadae wakaisambaza katika  vyuo vingine huko Marekani na mtandao ukawawezesha wanafunzi kuwasiliana na kutumiana picha kupitia mtandao huu na kabla hajaenda  Palo Alto,Califonia.

Mwaka 2007 Facebook ikampa utajiri mkubwa na kuwa miongoni mwa mabilionea ulimwenguni akiwa na umri wa miaka 23 tu.Hadi kufikia mwaka 2010 facebook ilikadiriwa kuwa na watumiaji  million 500 duniani na hadi kufikia mwaka 2012 facebook imekuwa na watumiaji  billion 1,na kumpa utajiri unaokadiriwa kufikia dola za kimarekani billion 9.4

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...