Friday, July 5, 2013

WALIMU 25 WALALAMIKIA FEDHA ZA UHAMISHO

  
 
Na  YEREMIAS  NGERANGERA----NAMTUMBO
                                                                               
 Wakati     serikali   ikiagiza   kuwa  uhamisho  wa  walimu  uendane na fedha za kugarimia uhamisho, kuepuka mzigo wa madeni kwa serikali , bado halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma iliwahamisha walimu 25 mwezi januari bila kuwalipa fedha zao mpaka sasa.. Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya walimu hao ambao hawakutaka majina yao yatajwe kwa ajili ya kuhofia ajira zao walisema kuwa walipata barua za uhamisho mwezi januari lakini chakushangazi waliambiwa walipoti vituo v ipya vya kazi  wakati taratibu za malipo yao zinaandaliwa. 

( Mimi toka Januari mwaka huu sijafundisha naendelea kusubiri fedha za uhamisho au gari la kubebea mizigo yangu Kutoka halmashauri na huu ni mwezi wa sita toka nipate barua ya uhamisho) alisema mwalimu mmoja. Baadhi ya walimu walidiriki kwenda kwa watu binafsi kwenda kukopa fedha kwa ajili ya kugharimia uhamisho huo kwa mategemeo ya kupata fedha toka kwa mwajiri kwa ajili ya kulipia madeni hayo wapo katika hali ya wasiwasi katika  vituo vyao vya kazi kutokana na kero za watu wanaowadai walimu hao. Hata hivyo  kuna baadhi ya walimu ambao hawakutaka kuingia hasara hiyo waliendelea kukaa nyumbani bila kufundisha kwa miezi sita mpaka shule zinafungwa w akisubiri fedha za uhamisho.

 Katibu wa chama cha walimu wilayani Namtumbo bwana Werner Mhagama aliwapongeza walimu walioendelea kusubiri fedha za uhamisho mara tu baada ya kwenda kuripoti kituo kipya na kurudi kituo cha awali kusubiri fedha za uhamisho au gari la kubebea mizigo yao kwa madai kuwa walimu hao wapo sahihi kwa kufuata kanuni za utumishi wa umma. Afisa elimu wa wilaya ya Namtumbo bwana Loberto Mbilinyi alikiri kuwepo kwa madai ya walimu hao na ku kusema kuwa madai hayo yanalipwa kwa awamu na baadhi ya walimu walisha lipwa. Mkurugenzi wa wilaya hiyo bwana Mohamed Maje alisema kuwa uhamisho wa walimu hao ulipita katika vikao halali kwa kwa lengo la kuboresha utendaji kazi na bajeti ya malipo kwa walimu hao ilishafanyika bali pametokea na uchelewaji wa fedha kutoka serikalini..

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...