Thursday, August 1, 2013

RAIA 9 NA ASKARI WAWILI WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA PEMBE ZA NDOVU

 Watu tisa wakiwemo wawili waliokuwa askari polisi wa kituo cha Osterbay jijini Dar es Salaam wamepandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Pwani wakituhumiwa kwa makosa mawili ya kukutwa na nyara za serikali na kushiriki katika kosa la kuhujumu uchumi kinyume cha sheria.
 
Kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba moja ya mwaka 2013 inaunguruma mbele ya hakimu mkazi nwandamizi mfawidhi wa mahakama hiyo Mh, Bahati Ndeserua,ambapo wakili wa serikali Bi Cecilia Shelly akisoma hati ya mashtaka mbele ya mahakama hiyo amewataja washtakiwa hao kuwa ni Koplo Senga Idd Nyembo,Pc issa Mtama,wengine ni Prosper Mareto,Seif Kadro,Said Kadro,wakazi wa panga la mwingireza vikumburu Kisarawe,Ramadhan Athmani,Musa Ali dereva mkazi wa Kinondoni studio ambaye kazi yake ni mgambo. Mahakama ikaambiwa kuwa,washtakiwa wote kwa pamoja wametenda makosa hayo Julai 28 mwaka huu katika kituo cha ukaguzi cha kauzeni na kijiji cha vikumburu Kisarawe mkoani Pwani,ambapo imedaiwa katika shtaka la kwanza washtakiwa hao walikutwa na nyara za serikali ambazo ni viapnde 70 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilo 306 vyenye thaamni ya shilingi milioni 850 na miatano mali ya serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania bila kuwa na kibali kutoka kwa mkurugenzi wa wanyama pori nchini. Katika shtaka la pili wakili wa serikali akaiambia mahakama kuwa,washtakiwa hao kwa pamoja walishiriki katika kosa la kuhujumu uchumi kinyume na sheria na kwamba wakiwa katika kijiji cha Vikumburu Kisarawe mkoani  Pwani kwa nia ya kutenda uovu walikutwa na nyara za serikali ambavyo ni vipande vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilo 306.5 vyenye thamani ya shilingi milioni 850 mali ya serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania bila kuwa na kibali kutoka kwa mkurugenzi wa wanyama pori nchini. Upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na washtakiwa  wote kwa pamoja hawakutakiwa kujibu lolote kisheria kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka kisheria ya kusikiliza kesi za aina hiyo na wamerudishwa rumande hadi Agosti 14, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena na upelelezi wa kesi mahakama imesema bado haujakamilika.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...