Thursday, August 1, 2013

TANZANIA NA THAILAND ZATILIANA SAINI MKATABA WA UHIFADHI WA MALI ASILI NA UTALII

.
WAZIRI MKUU WA THAILAND BI YINGLUCK SHINAWATRA AKISALIMIANA NA VIONGOZI MBALIMBALI
 Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na utalii imetiliana saini mkataba wa miaka mitatu wa ushirikiano katika uhifadhi wa mali asili na utalii na serikali ya Thailand ikiongozwa na waziri mkuu wake  Mh.  Yingluck Shinawatra.
Makubaliano hayo yamesasainiwa na waziri wa mali asili na utalii wa Tanzania kwa kumuhusisha naibu waziri  mkuu  wa Thailand Plodprasop Suraswad, mbele ya waziri  mkuu  huyo wa  Thailand kwa kuelezwa kuwa ni mwanzo mzuri katika kukuza sekta ya utalii nchini na kuchangia ukuaji wa uchumi. Akizungumza baada ya kutiliana saini katika mkataba huo,waziri wa mali asili na utalii Mh. Balozi Khamis  Kagasheki, amesema mbali na kukuza uchumi na utalii wa Tanzania, lakini pia makubaliano hayo yatasaidia kukuza kipato cha mtanzania kwani sekta ya utalii inachangia kwa asilimia 17 katika pato la taifa..
Kwa upande wake waziri wa uwekezaji na uwezeshaji nchini Mh Mary Nagu,amesema ujio wa waziri mkuu huyo wa Thailand hapa nchini kutawapa  fursa wawekezaji  wa  Thailand kuja kuwekeza nchini  katika sekta  mbalimbali.
Ziara hii ya siku moja ya waziri mkuu wa Thailand katika hifadhi ya taifa ya Serengeti ambao ni miongoni  mwa maajabu saba ya Afrika,imepokelewa kwa furaha kubwa na viongozi wa mkoa wa Mara na wadau  wa sekta ya utalii mkoani Mara.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...