Friday, September 13, 2013

MUNGU MKUBWA!!!!!!!! AUNT ASU AOKOKA,AACHANA KABISA NA MAMBO YA USHOGA

Aliyekuwa shoga maarufu aliyekuwa akijulikana kwa jina la anti asu ameokoka rasmi na kuachana kabisa na shughuli hiyo ambayo ni kinyume kabisa na maadili yetu ya kitanzania.

Blog hii ilianza kupata taarifa zake kwenye ukurasa wa instagram wa dida shaibu mtangazaji wa kipindi cha mitikisiko ya pwani wa kituo cha radio times fm.

Katika ukurasa wake huo dida ameandika aunt asu aacha ushoga amrudia mungu,na kuambatanisha picha kadhaa zikimuonesha aunt asu kabla hajaokoka na nyingine ikimuonesha baada ya kuokoka.

Aunt Asu alitangaza uamuzi wake huo katika kipindi cha mitikisiko ya  pwani cha kituo cha times fm ambapo huwa ni mahususi kwa kupiga nyimbo za taarabu na habari zinazuhusu wanamuziki wa taarab na wadau wa muziki huo hapa nchini na kinaendeshwa na mtangazaji huyo Dida Shaibu mwenye masham sham mengi katika kukichagiza.

Watu kadhaa wameonekana kutoa maoni yao tofauti wakimpongeza kwa hatua yake hiyo huku wengi wakisema ama kwa hakika mungu mkubwa na inapaswa woote wenye  tabia kama alizoziacha aunt asu waacha mara moja na kumrudia mungu.

Katika picha zilizooneshwa katika mtandao huo,wengi walionekana kutotambua kama aunt asu ni mwanamke au mwanaume kutokana na mavazi ya kike aliokuwa ameyavaa.
Lakini picha ya pili inamuonesha akiwa amevalia suti yu[po kanisani mara baanda ya kutangaza kuokoka.

Angalia picha zake hapa chini.

AUNT ASU KABLA HAJAOKOKA WAKATI AKIWA SHOGA
PICHA NYINGINE YA AUNT ASU
AUNT ASU KABLA HAJAOKOKA
BAADA YA KUOKOKA


NDANI YA SUTI BAADA YA KUOKOKA

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...