Friday, January 10, 2014

BASI LA MTEI EXPRESS LATEKETEZWA KWA MOTO NA WANANCHI BAADA YA KUWAGONGA NA KUUA WATOTO WATATU WA FAMILIA MOJA HUKO SINGIDA


DSC05595

DSC05594

DSC05596

DSC05599
DSC05601
Watoto watatu wa familia moja  ambao walikuwa wamepanda pikipiki wamekufa  baada ya kugongwa na basi  la Mtei express katika njia kuu itokayo Singida hadi Arusha ambapo baada  ya tukio hilo wananchi wenye hasira waliamua kulichoma moto basi hilo.

Kamanda wa polisi mkoani Singida  SACP Gefrey Kamwela  amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo imehusisha basi la Mtei  Express lenye usajili wa namba T 742 ACU lilikuwa likitokea Singida na kuelekea  jijini Arushana pikipiki aina ya Slag yenye usajili wa namba  T368 BXZ ambayo ilikuwa imepakia watoto watatu na baba yayo akiendesha.

Katika hatua nyingine kamanda Kamwella amewataja waliokufa papo hapo ni  Tabiri Shabani,Kasimu Shabani na Hamza Shabani kafa wakati akipatiwa matibabu na dereva wa pikipiki ambaye ni baba wa watoto hao  amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Singida.
Kwa upande wake shuhuda wa tukio hilo ambaye naye alikuwa abiria bwana Nakomolwa Thomas amesema dereva wa pikipiki aliamua kukata kona upande wa kulia bila ya kuangalia kama nyuma kuna basi lina kuja na kusababisha kugongwa na basi na kuburuzwa hadi pembeni mwa barabara.

Naye Nganga Mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Singida daktali Banuba Deogratius amesema wamepokea maiti mbili , mtoto moja amefariki wakati  wanampatia huduma na mwingine ambaye ni baba watoto hao bado anaendelea na matibabu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...