Wednesday, January 8, 2014

KICHANGA CHAOKOLEWA KUTOKA KWENYE TUNDU LA CHOO

Mtoto mchanga mwenye umri wa siku mbili amenusurika kufa baada ya mama yake mzazi, Hadija Pangani (29) Mkazi wa Kijiji cha Mpiruka Wilaya Nachingwea, Lindi kumfunga kwenye kiroba na kumtumbukiza chooni.
 
Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mpiruka, Simon Rashidi alisema mtoto huyo aligunduliwa na Techla Sameul baada ya kusikia sauti ya kulia alipokuwa anajisaidi kwenye choo hicho.
 
Simon alisema baada ya kusikia kelele za mtoto huyo, Techla alitoa taarifa kwa uongozi wa Serikali ya kijiji hicho, ambao kwa pamoja na kushirikiana na jamii na kufanikiwa kumwokoa mtoto huyo ambaye alikutwa hai akiwa amezungushiwa gagulo na kufungwa kwenye kiroba.
KWA HISANI YA EMMANUEL SHILATU BLOG

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...