Wednesday, July 2, 2014

IDADI YA WATU WALIOKUFA KATIKA AJALI YA NDEGE YA MIZIGO JOMO KENYATTA LEO ALFAJIRI WAFIKIA WA



254
Askari wa Jeshi la Kenya wakiwa eneo la tukio wakijaribu kutoa msaada katika Ndege ya mizigo iliyoanguka leo asubuhi katika eneo la Utawala kwenye Uwanja wa Jomo Kenyatta, jijini Nairobi.
Taarifa kutoka Kenya zinasema kuwa mpaka sasa imefahamika kuwa jumla ya watu wanne akiwamo Rubani, waliokua kwenye ndege hiyo wameripotiwa kufa baada ya ndege hiyo kuanguka dakika chache tu baada ya kupaa kutoka kwenye uwanja huo ikielekea Moghadishu, Somalia.
Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo ambapo imeelezwa kuwa ndege hiyo ilikua iondoke mapema kusafirisha zao la Mirungi na bidhaa nyinginezo kuelekea Somalia.
Akithibitisha ajali hiyo Mkuu wa Polisi wa Jiji la Nairobi, Benson Kibue, amesema kuwa kuwa Ndege hiyo yenye nambari 5Y-CET ilianguka kwenye paa la jengo la kibiashara wakati likijaribu kutua ghafla baada ya kutokea hitilafu katika ndege hiyo na kushika moto kisha kuanza kuteketea na watu wanne waliokua ndani.
Aidha kwa mujibu wa Mkuu wa Polisi wa Jijini Nairobi, Benson Kibue, amesema kuwa katika ajali hiyo walinzi wawili walijeruhiwa mmoja ametibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani huku mmoja akilalazwa katika hospitali ya Mama Lucy.
Polisi wanaendelea na uchunguzi kwenye mabaki ya ndege hiyo kuona iwapo kuna waathirika zaidi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...