Wednesday, August 28, 2013

WASIWASI WA UN KUHUSU MACHAFUKO CONGO

Umoja wa Mataifa umeelezea wasiwasi wake mkubwa kuhusiana na  kuongezeka machafuko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
 
Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, umoja huo una wasiwasi kuhusiana na kuongezeka mapigano baina ya jeshi la Congo DRC na wapigani wa waasi wa M23 huko mashariki mwa nchi hiyo. Farhan Haq amebainisha kwamba, usalama umevurugika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo baada ya kuzuka mapigano baina ya jeshi la nchi hiyo na waasi wa M23. Aidha amesema, Umoja wa Mataifa umeanzisha uchunguzi kuhusiana na kuuawa waandamanaji wawili mjini Goma, makao makuu ya jimbo la Kivu Kaskazini, maandamano ambayo yalifanyika kulaani mauaji dhidi ya raia pamoja na ukosefu wa amani mashariki mwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...