Saturday, September 14, 2013

RAISI WA ZANZIBAR ALLY MOHAMMED SHEIN AFIKA HOSPITALI KWENDA KUMUONA PADRI ALIYEMWAGIWA TINDIKALI


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Padre wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui, Joseph Mwang'amba, alipofika katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kumpa pole, Mjini Unguja, baada ya kumwagiwa tindikali Mjini Magharibi - Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Padre Joseph  Mwang'amba alipokuwa akitoa maelezo jinsi alivyopata mkasa wa kumwagiwa tindikali jana.
Mmoja wa Ndugu wa Padre aliyemwagiwa tindikali akimueleza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, hisia zake kwa uchungu kutokana na kitendo hicho cha kumwagiwa tindikali Padre na kuomba hatua zilichukuliwe ili kukomesha vitendo kama hivi ambavyo vimeanza kuzoeleka

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...